Na Innocent Natai, TPRI, Morogoro
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Kilimo
Mhandisi Mathew Mtigumwe, amewataka wakandarasi wa miradi ya Maghala na ujenzi
wa miundombinu ya umwagiliaji mkoani Morogoro kuhakikisha wanaikamilisha miradi
hiyo kwa wakati ili kuwasaidia wakulima na kuondoa changamoto za umwagiliaji na
uhifadhi wa zao la mpunga.
Mtigumwe ameyasema hayo wakati
akikagua utekelezwaji wa miradi ya ujenzi wa Maghala na ukarabati wa
miundombinu ya Umwagiliaji kijiji cha Mvumi wilayani Kilosa na Msolwa
Ujamaa wilayani Kilombero mkoani Morogoro,
Mradi unaojulikana kama Expanding Rice Production Project (ERPP) unaosimamiwa na Wizara ya
kilimo, wenye lengo la kusaidia kuongeza Uzalishaji kwa wakulima wadogo
wadogo wa Mpunga.
Mhandisi Mtigumwe amewataka
watendaji na wakandarasi kuhakikisha kuwa wanafanya haraka kukamilisha miradi
hiyo kabla ya muda uliopangwa wa kuisha kwa miradi hiyo mwezi wa nne mwaka 2020
kwani wananchi na wakulima wa mpunga wanaisubiri miradi hiyo kwa hamu ili kuwaondolea
changamoto ya umwagiliaji na uhifadhi.
‘’Kuna makontrakta ambao
mpaka sasa wapo nyuma kidogo katika ujenzi hasa wa ukarabati wa miundombinu ya
umwagiliaji lakini hawa wa maghala wapo vizuri wanaweza wakamaliza katika muda
uliopangwa hivyo ni jukumu lenu viongozi kuhakikisha tunawafuatilia hawa wa
umwagiliaji na mimi ntakuwa nakuja kila mwezi kuona wamefikia wapi na pia
wapewe barua za onyo haiwezekani muda wa mradi umekaribia kwisha alafu
mkandarasi bado anasuasua” Alisema Mhandisi Mtigumwe.
Alisema ni usaliti kwa Nchi
kupewa fedha za uzalishaji na ujenzi za ufadhili kutoka nje alafu baadhi ya
wakandarasi wazembe wanazitumia vibaya na kushindwa kuzipeleka katika matumizi
husika na kwa wakati husika bila kuchelewesha.
‘’Kabla miradi hii
kufikia katika hali mbaya nitawachukulia hatua kali za kisheria wakandarasi
wanaochelewesha miradi, siwezi kuvumilia kuona miradi mibovu na
inayocheleweshwa’’Aliongeza Mhandisi Mtigumwe
Ameongeza kuwa
utunzaji wa nafaka katika sekta ya Kilimo umekuwa ni changamoto
kubwa hivyo miradi hiyo ya maghala na umwagiliaji ikikamilika itasaidia katika
maeneo ya mradi, kuboresha mapato na nchi na kukuza uchumi kwa wakulima.
Kwa mujibu wa Mradi
huo Mhandisi January Kayumbe mradi huo umeletwa kwa ajili ya
kuimarisha zao la mpunga kwa wakulima wadogo kwa mkoa wa Morogoro na Zanzibar
ambapo umefadhiliwa na taasisi ya Global Agriculture & Food
Security Program (GAFSP) ambapo
wamefadhili dola za kimarekani takribani milioni 22.9 na ukisimamiwa na Benki
ya Dunia huku mtekelezaji wa mradi huu mkubwa akiwa ni Wizara ya Kilimo.
Katika usimamizi wa mradi
huu wizara tano zinahusika kwa upande wa Tanzania bara ikiwemo wizara ya Kilimo
ambayo ndio msimamizi mkuu, Viwanda na Biashara kwa ajili ya masoko, TAMISEMI
kwa sababu ya maeneo ya miradi inapotekelezwa yapo chini ya Halmashauri
na Wilaya ambazo zipo chini ya TAMISEMI, Wizara ya Maji kwa ajili ya kusimamia
hati za matumizi ya maji na Ofisi ya Makamu wa Rais mazingira kwa sababu
usimamizi wa mazingira ya ujenzi wa miundombinu ya miradi
Mradi huu ulianza mwaka
2015 na kwa ujenzi wa maghala ulianza mwaka huu mwezi Aprili katika maeneo
mbalimbali na unatarajiwa kukamilika Novemba mwaka huu na kwa upande wa
umwagiliaji ulianza mwezi Juni mwaka huu na uanatarajiwa kukamilika mwezi April
2020
MWISHO
0 comments:
Post a Comment