METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, October 21, 2019

NAIBU WAZIRI KANYASU AFUNGA MASHINDANO YA LIGI YA BASHUNGWA KARAGWE CUP


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akivishwa skafu na Daniel Ngwema Mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Mpira wa Kilimahewa kwa ajili ya kushuhudia fainali ya timu ya  Nyakahanga   dhidi ya timu ya Magambo katika mashindano ya ligi ya Bashungwa Karagwe Cup iliyofanyika katika wilaya ya Karagwe mkoani Kagera. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa wilaya hiyo, Mhe.Godfrey Mweruka akiwa pamoja na Waziri wa Biashara na Viwanda, Mhe.Innocent Bashungwa.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwa ameongozana na Mkuu wa wilaya ya Karagwe, Godfrey Mweruka akisalimiana na wachezaji wa timu Nyakahanga kabla ya mchuano huo kuanza katika uwanja wa Kilimahewa uliopp katika wilaya ya Karagwe mkoani Kagera.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akimkabidhi zawadi ya cheti mshangilia bora wa mashindano ya Ligi ya Bashungwa Karagwe Cup kabla kufunga mashindano hayo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akisaini kitabu cha wageni Mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Kilimahewa kushuhudia mechi kati ya timu ya Nyakahanga ambayo imeibuka kidedea katika ya timu ya Nyakahanga na Magambo. Wa pili Julia ni Waziri wa Biashara na Viwanda, Mhe.Innocent Bashungwa.
Baadi ya umati wa wakazi wa Karagwe waliojitokeza kushuhudia mechi kati ya Nyakahanga na Magambo ambapo Nyakahanga iliibuka kidedea kwa mikwaju ya penati.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu( Julia) akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza kushuhudia fainali ya mechi kati ya Nyakahanga na Magambo kabla ya kufunga ligi ya mashindano ya mpira wa miguu wa Bashungwa Karagwe Cup.
Vijana wa skauti wakipiga paradi mbele ya mgeni rasmi kabla ya fainali ya Bashungwa Karagwe Cup kuanza.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwa na viongozi wa mkoa wa Kagera wakiwa wameshika kombe kwa ajili ya kumkabidhi timu ya Nyakahanga iliyoibuka kidedea katika Mashindano ya Ligi ya Mpira wa miguu ya Bashungwa Karagwe Cup.
( Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii)
**********************************
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amefunga Mashindano ya  ligi ya mpira wa miguu ya Bashungwa Karagwe Cup ambapo timu  ya Nyakahanga imeibuka kidedea  dhidi ya timu ya Magambo.
 
Akizungumza kabla ya kufunga mashindano hayo,  Mhe.Kanyasu amewataka vijana kuitangaza Hifadhi ya Taifa ya Burigi-Chato kupitia  michezo
 
Naye, Waziri wa Biashara na Viwanda Mhe.Innocent Bashungwa ambaye ni Mbunge wa Karagwe na Mratibu wa Mashindano hayo amesema umati wa watu waliojitokeza kushuhudia Mashindano hayo ni ishara tosha ya umoja na mshikamano wa wakazi wa Karagwe kwa Mbunge wao
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com