METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, October 21, 2019

BADO GUGU VAMIZI NI KIZUNGUMKUTI KATIKA JIJI LA ARUSHA WADAU NA SERIKALI WAKUTANA






Na Innocent Natai, TPRI-Arusha

Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega amesemakuwa vita dhidi ya umaskini inahitajika kwenda sambamba na vita dhidi ya Gugu Karoti kwani linamadahara kwa afya ya binadamu,mimea na wanyama hivyo kuleta umaskini katika jamii hivyokurudihsha nyuma uchumi wa jamii.

Ameyasema hayo katika Mkutano wa wasiku ya gugu karoti uliofanyika Jijini Arusha na kukutanisha wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za serikali na binafsi ikiwa na lengo la kutafuta namna ya kukabiliana na gugu hilo ambalo linakuwa kwa kasi katika mkoa huo ili kujenga uelewa kwa jamii

Kwitega amesema wadau na wizara ya kilimo,mifugo, wataalam wa afya ya binadamu  na maliasili na utalii wanatakiwa kuunganisha nguvu kuhakikisha wanatokomeza ikiwa ni kuona ueneaji na usambaaji wa visumbufu hivi vamizi ili kuvitokomeza kwaajili ya kusaidia maisha ya binadamu wadudu na wanyama.

Pia amewataka kamati ya kutokomeza gugu hili kujenga uelewa wa kwa wadau wa kilimo,mifugo, wataalam wa afya ya binadamu  na maliasili na utaliiwa pia na mazingira ili kusaidia kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika kupiga vita gugu hili.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu vya kudhibiti visumbufu katika Ukanda wa Tropiki (Tropical Pesticides Research Institute-TPRI) Dr Esther Gwae Kimaro aliyewakilisha Mkurugenzi Mkuu

Amesema kuwa taasisi hiyo kupitia kwa watafiti wamejitahidi kuhakikisha wanakitokomeza kisumbufu hiki ikiwemo,kung’oa,na pia kwa kufanya tafiti mbalimbali na kumsambaza mdudu katika mikoa mbalimbali ambapo gugu hili limeonekana ukianzia na mkoani hapa Arusha ambae anakula gugu hili bila kuleta madhara kwa viumbe wengine na mazingira.

Pia kutoa elimu kwa wadau mbalimbali ikiwemo katika maonyesho mbalimbali mfano nanenane ili kuhakikisha wananchi wanalifahamu gugu hili na madhara yake katika mazingira na kwa wanyama.9 

Ramadhani Kilewa ni Mtafiti kitengo cha kidhibiti visumbufu vya mimea kutoka TPRI amesema kuwa Gugu karoti ni gugu hatari kwa wanyama na binadamu na kwasasa limeenea baadhi ya mikoa hapa nchini Tanzania ikiwemo mkoa wa Arusha hasa hasa katika maeneo mengi ya barabara na mashamba ya mazao.

Aidha amesemakuwa kamati ya kutokomeza Gugu karoti inakabiliwa na changamoto  ya rasilimali fedha ambapo ni tatizo kubwa kwani wakati wa kiangazi kuung”oa huo mmea inahitajika kutumia vitendea kazi vya ziada na pia usafiri kufika katika maeneo hayo.

‘’Tunaiomba serikali ya mkoa na wadau wengine kuungana nasi katika kudhibiti gugu hili katika jamii kwa ujumla Ofisi yako itusaidie kama tutapata hizo rasilimalifedha pia itusaidie kuwapa uelewa huu maafisa ugani,elimu ndiyo pekee ndiyo inaweza kuleta usawa kwa jamii kwa kuwaeleza juu ya gugu hili.’’ Alisema Kilewa

Jitihada za ziada zinahitajika katika kupambana na na gugu hili kwani ni hatari liliingia nchini haswa mkoa wa Arusha mwaka 2010 na linakuwa kwa kasi mno,linapunguza kuota kwa mazao,ni hatari kwa afya ya binadamu na wanayama ,inahatarisha maisha ya viumbe wengine,linaweza kusababisha jangwa,inasababisha pumu,na aleji ya ngozi kwa mujibu wa watafiti.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com