Na Maiko Luoga Ludewa
Mbunge wa Viti maalumu
kupitia chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Njombe, Dkt, Susan Kolimba amesimamia
zoezi la kuunda Vikundi vitano vya Wanawake wa chama hicho kutoka Tarafa tano
za Wilaya ya Ludewa kwa lengo la kuimarisha uchumi.
Zoezi la Kuunda vikundi hivyo
kutoka Tarafa tano za Liganga, Mawengi, Mlangali, Mwambao na Masasi limefanyika
katika ukumbi wa CCM wilaya ya Ludewa, wakati kikao cha Baraza la Wanawake wa
chama cha mapinduzi UWT wilayani humo likiendelea na Mgeni Rasmi alikuwa Dkt,
Susan Kolimba Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Njombe.
Akizungumza katika Kikao cha
Baraza la kawaida la UWT wilaya ya Ludewa kilichofanyika June 29/2019, Mgeni
Rasmi Dkt, Susan Kolimba aliwapongeza Viongozi wa UWT wilayani Ludewa kwa
kufanyakazi kwa bidii huku akiwashauri kuendelea kuonesha umoja na mshikamano
na jamii ili kujenga umoja, na upendo
Aidha Mbunge huyo ametoa
Fedha kiasi cha Tsh, 2,500,000/=
kwaajili ya kuviunga mkono Vikundi hivyo ambavyo kila kimoja kimepata Kiasi cha
Tsh, 500,000/= huku akitoa Wito kuwa, fedha hiyo itumike katika kuibua miradi
ambayo itawasaidia kujiletea maendeleo ya kweli na kuongeza chachu ya maendeleo
ya kiuchumi.
“Mmesema kuwa hamna vyanzo
vya Mapato kwaajili ya kujiimarisha kiuchumi, mimi nadhani leo hii mnatakiwa kuunda
Vikundi kila Tarafa kikundi kimoja ili muweze kufanya shughuli zenu za
uzalishaji mali, mimi leo nawakabidhi kiasi cha Tsh, 500,000/= kwa kila
kikundi” Amesema Dkt, Susan Kolimba Mbunge wa Viti maalumu CCM mkoa wa Njombe.
Dkt, Susan Kolimba kupitia
kikao hicho ameahidi kuendelea kusaidia Vikundi mbalimbali vya Wanawake
vilivyopo katika Tarafa zote za Mkoa wa Njombe, sambamba na kuwataka Wanawake
hao kuonesha Umoja na mshikamano katika kutekeleza majukumu yao ili kukuza
vipato vyao.
Kikao hicho cha Baraza la UWT
wilaya ya Ludewa kilifunguliwa na Mwenyekiti wake Bi, Leah Mbilinyi na
kuhudhuriwa na Mbunge mwingine wa Viti Maalumu mkoa wa Njombe kupitia CCM Mh,
Neema Mgaya pamoja na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ludewa Ndg, Stanley Kolimba.
Viongozi wengine Walioshiriki
Kikao hicho ni pamoja na Katibu wa CCM wilaya ya Ludewa Ndg, Bakari Mfaume,
Katibu wa UWT wilayani humo Bi, Flora Kapalia, Katibu wa UV,CCM wilaya Ndg,
Hassani Kapolo pamoja na Wajumbe wa UWT kutoka Kata zote 26 za Wilaya ya
Ludewa.
Baadhi ya Wajumbe
walioshiriki Kikao hicho wamempongeza na Kumshukuru Dkt, Susan Kolimba kwa
mchango wake wa mawazo, fedha na vifaa mbali mbali katika sekta ya afya, elimu
na uchumi anavyoendelea kutoa kwa wanawake na wananchi wote katika Mkoa wa
Njombe ili kuwasaidia waweze kuboresha huduma za kijamii, na vipato vyao.
0 comments:
Post a Comment