METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, June 5, 2019

WIZARA YA KILIMO IPO KWENYE MCHAKATO WA MABORESHO YA SERA YA TAIFA YA KILIMO-MHANDISI MTIGUMWE


Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Mhandisi Mathew John Mtigumwe

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Mhandisi Mathew John Mtigumwe anautangazia Umma wa watanzania kwamba Wizara ya Kilimo ipo kwenye mchakato wa maboresho ya Sera ya Taifa ya Kilimo ya Mwaka 2013. Maboresho haya yanalenga kuhuisha shughuli za kilimo ili ziendane na mahitaji halisi ya nchi ikiwa ni pamoja maendeleo ya viwanda.

Timu ya Wataalam ya Wizara ya Kilimo inaendelea na ukusanyaji wa maoni kutoka kwa Wadau maeneo mbalimbali ya nchi ikizingatia pia ushiriki wa makundi mbalimbali ya Kijamii.

Ili kutoa fursa kwa kila Mwananchi. Wizara inatoa wito kwa Wadau wote hasa wanaojihusisha na shughuli za kilimo, kutoa maoni, ushauri na michango yao na kushiriki katika mikutano hiyo; au kwa kupiga simu, kuandika barua na barua pepe kwa anwani zifuatazo:-

Katibu Mkuu,
Wizara ya Kilimo,
S.L.P 2182
40487 DODOMA.

Barua pepe: ps@kilimo.go.tz na dpp@kilimo.go.tz
Simu: 022-26 2321407

Tarehe ya mwisho ya kutoa maoni ni: - 30.06.2019

Taarifa hii imetolewa na:-
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
WIZARA YA KILIMO,
DODOMA,
04.06.2019
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com