Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini
Mhe.Antony Mavunde,akizungumza na uongozi wa Gereza la Msalato kabla ya
kukabidhi jezi kwa timu ya wafungwa Mashabiki wa Simba na Yanga
Timu za wafungwa wa Mashabiki wa Simba na
Yanga zikiingia uwanjani kupasha misuli kabla ya mechi kupiga ambapo
Mashabiki wa Simba wamewalaza wenzao wa Yanga 1-0 katika Gereza la
Msalato lilipo jijini Dodoma
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini
Mhe.Antony Mavunde,akikagua timu zote mbili za wafungwa Mashabiki wa
Simba na Yanga katika Gereza la Msalato kabla ya mpira kuanza.
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini
Mhe.Antony Mavunde,akitoa neno kwa timu zote mbili za wafungwa Mashabiki
wa Simba na Yanga katika Gereza la Msalato kabla ya mpira kuanza.
Kikosi cha Timu ya wafungwa wa Mashabiki
wa Simba wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya Mechi yao na wenzao wa
Yanga iliyopigwa uwanja wa Gereza la Msalato lililopo jijini Dodoma.
Kikosi
cha Timu ya wafungwa wa Mashabiki wa Yanga wakiwa katika picha ya
pamoja kabla ya Mechi yao na wenzao wa Simba iliyopigwa uwanja wa Gereza
la Msalato lililopo jijini Dodoma.
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini
Mhe.Antony Mavunde,akiingia uwanjani tayari kwa kufungua uzinduzi wa
mechi kati ya wafungwa Mashabiki wa Simba na Yanga katika Gereza la
Msalato kabla ya mpira kuanza.
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini
Mhe.Antony Mavunde,akipiga Penalti kwa kuashiria pambano la Mpira kati
ya wafungwa wa timu za Mashabiki wa Simba na Yanga katika Gereza la
Msalato kabla ya mpira kuanza.
Matukio katika picha timu zote mbili za
wafungwa Mashabiki wa Simba na Yanga wakichuana vikali Mechi ambayo
imepigwa katika uwanja wa Gereza Msalato jijini Dodoma ambapo Mashabiki
wa Simba wameibuka washindi wa goli 1-0.
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini
Mhe.Antony Mavunde,akiwa Meza Kuu na baadhi ya Viongozi akishuhudia
Mpira wa Miguu kati ya wafungwa Mashabiki wa Simba na Yanga katika
Gereza la Msalato ambapo Timu ya Mashabiki wa Simba wameibuka na ushindi
wa 1-0 dhidi ya wenzao wa Yanga.
Mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini Mh.Antony
Mavunde,akikabidhi zawadi ya dawa ya meno kwa Nahodha wa Kikosi cha
Timu ya Wafungwa wa Mashabiki wa Yanga katika mechi ambapo Mashabiki wa
Simba wameibuka Kidedea kwa ushindi wa bao 1-0 katikati ni Mbunge wa viti maalum Mariam Ditopile
Mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini Mh.Antony
Mavunde,akikabidhi ya Kombe pamoja na Mpira kwa Nahodha wa Kikosi cha
Timu ya Wafungwa wa Mashabiki wa Simba katika mechi ambapo Mashabiki wa
Simba wameibuka Kidedea kwa ushindi wa bao 1-0 katikati ni Mbunge wa viti maalum Mariam Ditopile.
Picha na Alex Sonna-Wazo huru blog
………………..
Na.Alex Mathias,Dodoma
Timu ya wafungwa mashabiki wa Simba
katika Gereza la Msalato Jijini Dodoma imeibuka na Ushindi wa 1-0 dhidi
ya timu ya Mashabiki wa Yanga mchezo uliopigwa katika uwanja wa Gereza
hilo ukihudhuliwa na viongozi mbalimbali pamoja na wananchi wa kanda
hiyo.
Mechi hiyo iliyochezwa katika sikukuu ya Idd pili ikiwa ni hitimisho la
Bonanza lililoandaliwa na Mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini Mh.Antony
Mavunde ilianza majira ya saa sita kamili za Mchana,
Timu zote zilianza kwa kushambuliana kwa
kasi kubwa katika dakika ya 30 timu ya mashabiki wa Simba wakikosa
Penalti baada ya mpigaji kupiga shuti nje ya goli.
Mnamo dakika ya 35 mshambuliaji wa timu
ya mashabiki wa Simba,Maneno Mwang,ona aliwanyanyua mashabiki wake kwa
kufunga bao safi kwa mpira wa Faulo ulioenda moja kwa moja na kumshinda
mlinda mlango wa Yanga.
Hadi timu zikienda katika mapumziko Mashabiki wa Simba walikuwa wanaogoza bao 1-0 kwa bila.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote mbili kufanya mabadiliko ambayo yaliwasaidia zaidi Mashabiki wa Simba kulinda bao lao.
Mnamo dakika ya 80 timu ya Mashabiki wa
Yanga walikosa Penalti baada ya kuchezaji wao kupiga nje ilitokana na
beki wa Simba kumchezea Rafu na mwamuzi kuamua kuwa tuta hata hivyo
alikuzaa matunda.
Hadi Mwamuzi anapuliza kipyenga cha mwisho timu ya Mashabiki wa Simba wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya watani zao Yanga.
Kwa Ushindi huo Timu ya Mashabiki wa
Simba wametwaa ubingwa wa bonaza hilo na kukabidhiwa zawadi mbalimbali
wamekabidhiwa kutoka kwa Mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Antony
Mavunde.
Mhe.Mavunde alikuwa mgeni rasmi wa Bonanza hilo,kwa pamoja amekabidhi
zawadi ya Jezi kwa timu zote mbili,sabuni,dawa ya Meno pamoja na Kikombe
kwa Timu iliyoshinda ambapo pia ametoa rai kwa watanzania wote kujenga
utamaduni wa kuwasaidia watu wenye uhitaji ikiwemo wafungwa kwani ni
moja ya sadaka.
“Nitoe wito kwa watanzania wote hasa katika sikukuu hizi,kujenga
utamaduni wa kuwasaidia watu wenye uhitaji kama hawa,kwani hiyo ni moja
wa Sadaka,watu hawa japo ni wafungwa lakini jamii bado inawahitaji,nami
nitaendelea kuja kwa kadri ntakavyohitajika”amesema Mavunde
Kwa upande wao uongozi wa Gereza hilo wao wamekiri kufarijika na
kumshukuru Mbunge Mavunde pamoja na wabunge wote kwa ujumla waliojitolea
kuwapeleka vitu mbalimbali wakati wote wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa
Ramadhani.
0 comments:
Post a Comment