METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, June 10, 2019

LUKUVI AKUTANA NA BUTIKU KUJADILI USHIRIKIANO

*********************************************
Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi leo tarehe 10 Juni 2019 amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku kujadiliana masuala mbalimbali ikiwemo namna Wizara hiyo itakavyoshirikiana na Taasisi ya Mwalimu Nyerere katika maeneo yanayohusu wananchi.
Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisi za Wizara zilizopo eneo la Mtumba jijini Dodoma, Butiku alitumia fursa ya kukutana na Waziri Lukuvi kumuelezea kazi za taasisi yake hasa katika kushughulikia Amani, Umoja na Maendeleo ya watu.
Pia Mkurugenzi huyo wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere alimueleza Lukuvi kuhusu ufunguzi wa Jengo la Taasisi yake la Ghorofa 30 liliko Dar es Salaam ambalo linatarajiwa kufunguliwa mwanzoni mwa  mwezi Agosti 2019 ambapo uzinduzi wake utaenda sambamba na sherehe za kumuenzi na kumbukumbu ya Baba wa Taifa miaka 20 baada ya kifo chake.
Kwa mujibu wa Butiku wakati wa ufunguzi wa jengo hilo pia kutafanyika Kongamano la Kimataifa kuhusu kazi za Taasisi ya Mwalimu ikuhusisha Amani,Umoja na Maendeleo yenye tija kwa watu wote huku msisitizo ukiwa katika utekelezaji wa sera ya kwenda katika nchi yetu.
Kupitia kikao hicho, Butiku alipata ushauri kuhusu maeneo ambayo Taasisi ya Mwalimu Nyerere ingependa hasa maeneo yanayohusu wananchi moja kwa moja vijijini na mijini na ambayo ni muhimu kwa amani umoja na maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake Waziri Lukuvi alimshukuru Butiku kwa kumtembelea kwa lengo la kupata ushauri hasa katika masuala yanayohusu wananchi na kueleza kuwa kikao chao mbali na kubadilishana uzoefu  lakini pia kililenga katika kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo huku msisitizo ukiwa ni kuleta Amani  na Umoja kwa taifa kwa ujumla.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com