METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, March 26, 2019

WIZARA YA KILIMO KUINGIA MAKUBALIANO YA KUSHIRIKIANA NA TBL KUIMARISHA MASOKO YA WAKULIMA – MHE BASHUNGWA

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika nchi za Tanzania na Uganda Ndg Philiph Redmaw baada ya kukutana na kufanya mazungumzo leo tarehe 26 Machi 2019, Jijini Dodoma. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Baadhi ya watendaji wakifatilia kikao kazi cha Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika nchi za Tanzania na Uganda Ndg Philiph Redmaw leo tarehe 26 Machi 2019, Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) akisisitiza jambo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika nchi za Tanzania na Uganda Ndg Philiph Redmaw leo tarehe 26 Machi 2019, Jijini Dodoma.
Baadhi ya watendaji wakifatilia kikao kazi cha Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika nchi za Tanzania na Uganda Ndg Philiph Redmaw leo tarehe 26 Machi 2019, Jijini Dodoma.

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo – Dodoma

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika nchi za Tanzania na Uganda Ndg Philiph Redmaw kujadili namna ya kufungamanisha uchumi kupitia sekta ya Kilimo na Viwanda.

Akizungumza katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano maarufu kama Kilimo (IV) Jijini Dodoma leo tarehe 26 Machi 2019, Mhe Bashungwa alisema kuwa kampuni hiyo inazalisha bia kwa wingi nchini Tanzania hivyo makubaliano hayo yanaongeza chachu na tija katika kuongeza masoko ya wakulima nchini.

Kwa kauli moja kikao hicho kimeridhia mkataba huo kusainiwa mwezi Aprili mwaka huu “Tutasaini mkataba wa makubaliano kati yetu serikali na kampuni ya TBL ili kuimarisha soko la wakulima kwani TBL wanategemea bidhaa zitokanazo na mazao ya mtama, zabibu, shairi na mahindi” Alisema

Katika kikao hicho Mhe Bashungwa amesema kuwa makubaliano hayo punde yatakaposainiwa yataongeza mtazamo wa jumla kwa wakulima nchini kujipatia masoko ya mazao hayo ya mvinyo.

Katika zaao la mahindi pekee nchini wakulima wana ziada ya Tani 810,000 huku bei ikiwa chini hivyo makubaliano hayo yametazama zaidi mahitaji ya TBL kwenye mahindi na kuzingatia ubora ili wakulima waweze kunufaika na fursa hiyo” Alikaririwa Mhe Bashungwa

Alisema kuwa moja ya mikakati ya serikali ya awamu tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli ni pamoja na kutafuta masoko ya mazao ya wakulima nchini ili wakulima wa mazao yote waweze kunufaika na utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

“Tumeamua kuingia makubaliano na TBL kwa kuwa katika kipindi cha muda mrefu wakulima wamekuwa wakihakikishiwa na kampuni za vinywaji kulima mazao mengi kwamba soko lipo lakini baada ya mavuno kampuni zinaingia mitini bila manufaa kwa wakulima wetu, sasa hatutaki kurudi huko huu ni mkakati kabambe wa kuwanufaisha” Alikaririwa Mhe Bashungwa

Makubaliano hayo yatabainisha majukumu ya kila mmoja ndani ya TBL na wizara ya kilimo ambapo Benki ya Maendeleo ya kilimo (TADB) kutoa ushirikiano kwa mkulima kuanzia hatua za awali za uzalishaji mbegu kwenda kwa mkulima sambamba na elimu kutolewa kwa mkulima kuhusu kuzingatia kanuni bora za kilimo.

Alisema kuwa kikao hicho pia kimetazama namna ambavyo TADB itaweza kusaidia Wakala wa Mbegu Tanzania (ASA) ili kuzalisha kwa wingi mbegu bora zitakazosambazwa kwa wakulima ili wakulima hao waweze kuzalisha mazao bora na yenye tija katika soko.

Bashungwa amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kuakisi utendaji na mkakati wake wa kuimarisha masoko ya wakulima nchini.

MWISHO
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com