Na Munir Shemweta, WANMM Kilimanjaro
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo
ya Makazi Mhe. William Lukuvi amekata mzizi wa fitna ambapo ameagiza waliokuwa
wafanyakazi wa chama cha ushirika katika eneo la Lambo Estate Wilaya ya Hai
Mkoa wa Kilimanjaro kutoondolewa katika eneo hilo na kila mmoja kupatiwa ekari
mbili kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za kimaisha.
Uamuzi huo wa Lukuvi wa kutoa
ekari mbili kwa wananchi hao 78 unafanya kutolewa kwa jumla ya ekari 156
kati ya ekari 1600 . Uamuzi huo unafuatia mgogoro wa muda mrefu baina ya
waliokuwa wafanyakazi wa ushirika na uongozi .Mgogoro huo umeibuka baada ya
wafanyakazi hao kutakiwa kuondoka katika makazi yaliyopo kwenye eneo la
shamba kutokana na utumishi wao kukoma.
Waziri Lukuvi alitoa maamuzi hayo leo
katika wilaya Hai ikiwa ni mwanzo wa ziara yake ya kutembelea wilaya za
Hai, Moshi na Same kushughulikia migogoro ya ardhi katika wilaya hizo mkoa wa
Kilimanjaro.
Mhe Lukuvi ameshangazwa na ushirika
wa watu wachache kutaifisha ardhi na kuamuru watu waliokuwepo muda mrefu katika
eneo la lambo estate kuondoka na kusema kuwa safari hii serikali itawanyoosha
wale wote wanaofanya ujanja wa kuwaonea wanyonge.
*"Sijawahi kuona ushirika wa
namna hii ambapo wenye rasilimali hawanufaiki na ardhi iliyopo katika
kijiji chao halafu ardhi hiyo inakodishwa kwa wanachama wa ushirika
wanaotoka vijiji vingine"* alisema Waziri Lukuvi.
Huku akishangiliwa na wananchi wakati
akitoa maamuzi hayo, Mhe. Lukuvi alisema amekwenda katika eneo hilo la
Lambo Estate kushughulikia mgogoro wa ardhi. Suala la ushirika litashughulikiwa
na waziri mwenye dhamana na vyama vya ushirika ambae ataamua iwapo
ushirika huo unafaa. Waziri Lukuvi alisisitiza kuwa, serikali haiwezi kuwaondoa
wazee walioishi kwa muda mrefu.
Waziri wa Ardhi ametoa maagizo kwa
wananchi watakaopewa ekari mbili kuwa maeneo watakayopatiwa ni kwa ajili ya
kufanyia shughuli zao na hawaruhusiwi kuuza na kwa yeyote atakayeamua kuondoka
eneo hilo basi eneo hilo litabaki kuwa la serikali.
Kufuatia maelekezo hayo Mkuu wa
Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya
ya Hai kuanza mara moja zoezi la kuwagawia wananchi ekari hizo kama
ilivyoagizwa na mhe Lukuvi.
Awali Katibu wa jumuiya ya
wanaushirika Edward Chedi alimueleza Mhe Waziri Lukuvi kuwa mgogoro wa eneo
hilo ulianza mara baada ya shamba hilo kutaifishwa na ajira za walikuwa
wafanyakazi wa ushirika kukoma mwaka 2001 na kuwepo mfululizo wa kesi uliofikia
ngazi ya Mahakama Kuu na kuagizwa waliokuwa wafanyakazi kulipwa mafao na
kukabidhiwa vyeti vya kutambuliwa pamoja na ekari hamsini za kujikimu kwa
kipindi watakachokaa hapo kabla ya kuondolewa.
---------------------------------MWISHO----------------------------------------------------
CAPTION ZA PICHA
PIX NO 4438, - Waziri wa Ardhi Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimsikiliza Meneja wa Kiwanda cha
Kilimanjaro Machine Tools Manufacturing Co Ltd cha eneo la Viwanda la Weruweru
wilaya ya Hai Andreano Nyaluke wakati wa ziara ya kushughulikia migogoro ya
ardhi katika mkoa wa Klimanjaro.
PIX NO 4440, 4448, 4468- Waziri wa
Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimsikiliza Meneja wa
Kiwanda cha Kilimanjaro Machine Tools Manufacturing Co Ltd cha eneo la Viwanda
la Weruweru wilaya ya Hai Andreano Nyaluke wakati wa ziara ya kushughulikia
migogoro ya ardhi katika mkoa wa Klimanjaro.
PIX 4441-Baadhi ya wananchi wa eneo
la Shamba la Lambo Estate katika wilaya ya Hai mkoa wa Kilimanjaro wakifurahia
baada ya Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutoa maagizo wananchi
hao wasiondoke katika eneo hilo sambamba na kila mmoja kupatiwa ekari mbili kwa
ajili ya kufanyia shughuli zao.
PIX NO 4443- Baadhi ya wananchi wa
eneo la Shamba la Lambo Estate katika wilaya ya Hai mkoa wa Kilimanjaro
wakifurahia baada ya Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutoa
maagizo wananchi hao wasiondoke katika eneo hilo sambamba na kila mmoja
kupatiwa ekari mbili kwa ajili ya kufanyia shughuli zao.
PIX NO 4448-Waziri wa Ardhi Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akipata maelezo ya mashine
iliyotengenezwa katika Kiwanda cha Kilimanjaro Machine Tools
Manufacturing Co Ltd cha eneo la Viwanda la Weruweru wilaya ya Hai kutoka kwa
meneja wa kiwanda hicho Andreano Nyaluke wakati wa ziara ya kushughulikia
migogoro ya ardhi katika mkoa wa Klimanjaro.
PIX NO 4486, 4494, 4502- Baadhi ya
nyumba za wananchi waliokuwa wafanyakazi wa Ushirika katika eneo la Lambo
Estates wilaya ya Hai mkoa wa Kilimanjaro ambao Waziri wa Ardhi Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi aliamuru wasiondoke eneo hilo na
kuwapatia kila mmoja ekari mbili kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao ikiwa ni
utatuzi wa mgogoro wa muda mrefu.
PIX NO 4510- Baadhi ya wananchi
waliokuwa wafanyakazi wa Ushirika katika eneo la Lambo Estates wilaya ya
Hai mkoa wa Kilimanjaro wakimsikiliza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya
Makazi Mhe. William Lukuvi ambaye aliamuru wasiondoke eneo hilo na kuwapatia
kila mmoja ekari mbili kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao ikiwa ni utatuzi wa
mgogoro wa muda mrefu. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)
0 comments:
Post a Comment