METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, October 11, 2018

SERIKALI YASISITIZA KUUFUNGA MGODI WA KOKOTO BAGAMOYO


Naibu Waziri wa Madini, Mwl. Doto Mashaka Biteko amefika katika machimbo (mgodi) ya kokoto Lugoba,  Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani na kuridhishwa na utendaji kazi katika machimbo hayo.

Mwl. Biteko ametoa pongezi kwa kampuni ya Yaate Investment kwa kushirikiana na kampuni ya Yapi Merkezi kwa uwekezaji mzuri unaozingatia sheria ya madini.

Akiwa katika machimbo hayo, ametoa muda usiozidi siku tano hadi jumatatu wiki ijayo kwa Bw. Akram Aziz ambaye ametelekeza mitambo/ vifaa yake ya uchimbaji kokoto katika eneo hilo vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake kwani ni kosa kisheria kutelekeza mitambo hiyo kwenye eneo la leseni ya uchimbaji lisilo lake.

Ifahamike kwamba malighafi za ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge Railway) zinatoka katika mgodi huo.

Katika hatua nyingine, Mwl. Biteko ametoa msimamo wa serikali wa kuendelea kuufunga mgodi wa kokoto unaomilikiwa na kampuni ya Lugoba Tan-Turk Stone Quarry hadi utakawalipa fidia wakazi wanaozunguka mgodi huo ili wapishe shughuli kuendelea.

Uongozi wa mgodi huo kupitia kwa Mkurugenzi wake, Raci Omary umeomba kupewa muda hadi mwezi Disemba mwaka huu ili kutoa fidia kwa wakazi hao.
Sehemu ya mchanga na kokoto katika mgodi wa kokoto Yaate Investment
Sehemu ya mchanga na kokoto katika mgodi wa kokoto Yaate Investment
Naibu Waziri wa Madini, Mwl. Doto Biteko akikagua mgodi wa Lugoba Tan-Turk Stone Quarry ambao umefungiwa.
Naibu Waziri wa Madini, Mwl. Doto Biteko akikagua eneo la upasuaji kokoto katika mgodi wa Lugoba Tan-Turk Stone Quarry
Sehemu ya mitambo iliyotekelezwa katika eneo la mgodi wa upasuaji kokoto wa Yaate Investment

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com