METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, October 24, 2018

MJUMBE WA KAMATI KUU CCM TAIFA, MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MKUTANO WA KAMPENI JIMBO LA JANG`OMBE

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa mkutano wa kumnadi mgombea wa Uwakilishi jimbo la Jang`ombe kwenye viwanja vya Baja. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Dkt. Abdulla Juma Sadala wakati wa mkutano wa kumnadi mgombea wa Uwakilishi jimbo la Jang`ombe kwenye viwanja vya Baja. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi pamoja na Katiba ya Chama mgombea wa CCM nafasi ya Uwakilishi Jimbo la Jang`ombe Bw. Ramadhan Hamza Chande wakati wa mkutano wa kumnadi mgombea wa Uwakilishi jimbo la Jang`ombe kwenye viwanja vya Baja. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo alikuwa mgeni rasmi katika mkutano wa kampeni jimbo la Jang`ombe ambapo Chama Cha Mapinduzi kimemsimamisha Bw. Ramadhan Hamza Chande kugombea nafasi ya Uwakilishi katika jimbo hilo.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa, Makamu wa Rais amewataka wakazi wa Jang`ombe kufuata nyayo walizoachiwa na Wazazi wao.
Mheshimiwa Samia amewambia wakazi wa jimbo hilo kuwa atatoa ushirikiano wa kutosha kwa kufanya kazi pamoja na Viongozi wa Jimbo hilo katika kuboresha huduma za afya na elimu.
Pamoja na Viongozi wengine Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Mbunge mteule wa jimbo la Liwale kutoka mkoani Lindi Bw. Zuberi Kachauka ambaye aliwaambia wakazi wa Jimbo la Jang`ombe kuwa upinzani umekufa kwa kukosa sera na viongozi bora.
Kampeni za Uwakilishi jimbo la Jang`ombe zilianza tarehe 14 Oktoba na zinatazamiwa kukamilika tarehe 25 Oktoba  2018 na tarehe 27 Oktoba wananchi watapiga kura kumchagua Mwakilishi wa jimbo hilo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com