METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, February 26, 2018

MAAFISA WA SERIKALI WANAONYANYASA WACHIMBAJI KUCHUKULIWA HATUA

Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko (Kushoto) akifurahi jambo na Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini Mhe Dkt. Khamis Kigwangala mara baada ya kutembelea uliopokuwa mgodi wa Dhahabu wa Resolute katika kijiji cha Isanga kilichopo Kata ya Lusu Wilayani Nzega, Leo 26 Februari 2018. Picha Na Mathias Canal-Wazo Huru Blog
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko pamoja na mwenyeji wake Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini Mhe Dkt. Khamis Kigwangala wakikagua uliopokuwa mgodi wa Dhahabu wa Resolute katika kijiji cha Isanga kilichopo Kata ya Lusu Wilayani Nzega, Leo 26 Februari 2018. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua baadhi ya ofisi za Kampasi ya Chuo cha Madini Dodoma (MRI) kwenye eneo lililokuwa mgodi wa Dhahabu wa Resolute katika kijiji cha Isanga kilichopo Kata ya Lusu Wilayani Nzega, Leo 26 Februari 2018. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko pamoja na mwenyeji wake Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini Mhe Dkt. Khamis Kigwangala wakikagua uliopokuwa mgodi wa Dhahabu wa Resolute katika kijiji cha Isanga kilichopo Kata ya Lusu Wilayani Nzega, Leo 26 Februari 2018. 

Na Mathias Canal, Tabora

Serikali imebainisha kuwa zipo taarifa za maafisa wa serikali waliopewa dhamana ya kusimamia sekta ya madini lakini wamekuwa kikwazo kwa kuwa na usumbufu mkubwa wa manyanyaso kwa wachimbaji wadogo nchini.

Unyanyasaji huo unajili wakati ambapo wachimbaji hao wametumia nguvu na muda wao mwingi na hatimaye kujipatia Madini lakini kabla ya kuuza maafisa mbalimbali wa serikali hususani katika sekta ya Madini huingiza kikwazo kwa madai ya kuhitaji mgao Mara baada ya mauzo.

Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko amesisitiza hayo wakati akiwa katika ziara za kikazi katika Mkoa wa Rukwa, Katavi na Tabora ambapo amewataka maafisa hao kuacha Mara moja kadhia hiyo kwanini kufanya hivyo ni kwenda kinyume na taratibu na sheria za utumishi wa umma.

Leo 26 Februari 2018 akiwa katika Kijiji cha Isanga kilichopo katika Kata ya Lusu Wilayani Nzega akizungumza na wananchi ambao asilimia kubwa ni wachimbaji wadogo katika eneo ambalo ulikuwa mgodi wa Dhahabu wa Resolute, Mhe Biteko aliwasihi wachimbaji hao kuwa wavumilivu wakati serikali inafanya utaratibu bora katika sekta ya Madini ili kuwa na uchimbaji wenye tija.

Mhe Biteko akiwa katika eneo hilo ambalo kwa sasa ni Kampasi ya Chuo cha Madini Dodoma (MRI) alisema kuwa serikali haitatoa ruzuku kwa wachimbaji wadogo badala yake itatoa wataalamu na Vifaa vya Utafiti ili kubaini maeneo yenye Madini na hatimaye wananchi kuchimba maeneo yenye uhakika wa rasilimali hiyo.

Katika hatua nyingine rungu limewaangukia Wamilili wa Leseni za Madini ambao hawajayaendeleza maeneo yao ambapo alisema kuwa serikali inaendelea kujiridhisha pindi itakapomaliza ufuatiliaji wake itawaandikia hati ya makosa kisha kuwafutia maeneo hayo kwa ajili ya kuwakabidhi wachimbaji wadogo.

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini Mhe Dkt. Khamis Kigwangala amewahakikishia wananchi wa jimbo hilo kuwa serikali ya awamu ya tano imekusudia kuwanufaisha wananchi kupitia rasilimali mbalimbali ikiwemo madini hivyo ziara ya Naibu Waziri Mhe Doto Mashaka Biteko nitakuwa na tija kwani amejionea uhitaji wa maeneo kwa wachimbaji wadogo.

Aidha, aliwasisitiza Wachimbaji hao pindi serikali itakapotoa ruhusa ya maeneo yao ya kuchimba kuzingatia Sheria na Taratibu ili kuwa na uchimbaji wenye tija na uzalishaji mkubwa.

MWISHO.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com