METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, February 24, 2018

Dkt. Mwanjelwa apiga marufuku Madalali wa Mazao kunyonya Wakulima

  Naibu Waziri Kilimo Dkt. Mary Mwanjelwa akizungumza na Wakulima wa nyanya katika Kijiji cha Ugwachanya mapema leo

  Naibu Waziri Kilimo Dkt. Mary Mwanjelwa akishangiliwa na wakina Mama Wakulima wa nyanya katika Kijiji cha Ugwachanya mapema leo

Naibu Waziri wa Kilimo Dkt. Mary Mwanjelwa amepiga marufuku madadali wanaojihusisha na biashara ya mazao ya kilimo kuwanyonya Wakulima kote nchini na kusisitiza kuwa Serikali haitakaa iwavumilie kwani kuwanyonya Wakulima ni kosa kama yalivyo makosa mengine.

Dkt. Mwanjelwa ameyasema hayo mapema leo katika mkutano na Wakulima wa zao la nyanya wa Kijiji cha Ugwachanya Kata ya Mseke na Tarafa ya Mlolo mara baada ya kupokea risala ya Wakulima wa nyanya ambao wamemweleza kutoridhishwa na mwenendo wa Kampuni ya Darsh ambayo imekuwa ikinunua nyanya za Wakulima hao kwa shilingi 150 kwa kilomoja.

Naibu Waziri huyo amesema malipo ya shilingi 150 kwa kilo moja ya nyanya yapo chini sana na kuuagiza Uongozi wa Kampuni ya Darsh kurekebisha kasoro hiyo.

Naibu Waziri huyo hakusita kuwaeleza wazi wazi namna ambayo Serikali inavyokerwa na vilio vya Wakulima kuhusu bei za mazao kuwa chini huku kukiwa na juhudi za makusudi za kuwalalia Wakulima kwa visingizio mbalimbali.

“Nataka kila Mkulima afahamu kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli lengo lake ni kumuinua Mkulima na kama kuna aina ya unyonyaji wa aina hii ya kuwalalia Wakulima, haitasita kumchukulia hatua.

Kampuni ya Darsh ilihamasisha Wakulima wa Kijiji cha Ugwachanya kulima nyanya kwa wingi katika msimu wa kilimo ya 2016/2017 ambapo katika Kata ya Mseke Jumla ya ekari 185 zililimwa na hali hiyo ilichangia uzalishaji mkubwa na kinyume cha matarajio ya Wakulima Kampuni hiyo haikununua nyanya sawasawa na mkataba wa awali.

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com