METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, February 17, 2018

DC MTATURU AWATAKA WANANCHI KUZINGATIA KANUNI ZA UHIFADHI BWAWA

 Afisa uvuvi wilaya Josephine Mazula  akimuonyesha mkuu wa wilaya ya Ikungi Miraji Mtaturu vifaranga  vya samaki vipataavyo 3,500 vyenye thamani ya shilingi laki  9 vilivyopatikana Kingorowira Morogoro.
Mkuu wa wilaya ya Ikungi Miraji Mtaturu akisalimiana na afisa uvuvi wilaya Josephine Mazula wakati akionyeshwa vifaranga vya samaki vilivyotoka Kingorowira Morogoro.

MKUU wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida mhe. Miraji Mtaturu amewataka wananchi kufuata kanuni za uhifadhi mabwawa kwa  kutofanya shughuli za kilimo na ufugaji mita 60 pembezoni mwa bwawa.

Mtaturu ametoa agizo hilo wilayani humo wakati wa zoezi la upandaji miti baada ya agizo lake la kupandikizwa upya kwa vifaranga vya samaki katika bwawa la Muyanji lililopo katika kijiji cha Kimbwi kata ya Makiungu  kutekelezwa.

Katika agizo lake hilo alilowahi kulitoa mwishoni mwa mwaka jana alipotembelea bwawa hilo alimuelekeza mkurugenzi wa halmashauri hiyo kutafuta vifaranga vipya ili kuongeza uchumi kwa wananchi baada ya kuelezwa kuwa samaki wamepungua na wanaovuliwa ni wadogo sana.

Akizungumza katika zoezi hilo la upandaji miti mheshimiwa Mtaturu amewaelekeza wananchi kuwa bwawa hilo litafungwa kwa miezi 6 hadi mwezi agosti mwaka huu ili samaki wafikie kiwango kinachotakiwa kuvuliwa.

"Tunajua bwawa hili tukilitumia vizuri na kufuata kanuni za uhifadhi wake tutaongeza uchumi wetu,na kwa kutambua umuhimu wa bwawa hili mpango wa halmashauri wa baadae ni kuongeza kina na kutenga bajeti katika mwaka wa fedha wa 2018/2019,"alisema Mtaturu.


Bwawa hilo linaajiri wavuvi zaidi ya 3,000 ambao wanafanya shughuli mbalimbali za kiuchumi.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com