METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, September 21, 2017

MBALI NA MBEGU ZA MAHARAGWE WAKULIMA WAOMBA MRADI WA N2AFRICA KUWAPATIA MBEGU ZA MAZAO MENGINE

Mkulima wa zao la maharagwe Kitongoji cha Dukani, Kijiji na Kata ya Baga, Wilaya ya Bumbuli Ndg Ismail Abasi akionyesha mbuzi wa maziwa aliowanunua kutokana na mafanikio mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe.
Wataalamu wa utafiti kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa kilimo cha Kitropiki (IITA) wakimsikiliza Mkulima wa zao la maharagwe Kitongoji cha Dukani, Kijiji na Kata ya Baga, Wilaya ya Bumbuli Ndg Ismail Abasi akielezea mafanikio aliyoyapata kutokana na mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe.

Mkulima wa zao la maharagwe Kitongoji cha Dukani, Kijiji na Kata ya Baga, Wilaya ya Bumbuli Ndg Ismail Abasi akionyesha Ng'ombe wa maziwa aliowanunua kutokana na mafanikio mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe.
Mwandishi wa habari Mwandamizi na Mhariri wa Mtandao wa www.wazo-huru.blogspot.com Ndg Mathias Canal (Kulia) alipomtembelea Mkulima wa zao la maharagwe Kitongoji cha Dukani, Kijiji na Kata ya Baga, Wilaya ya Bumbuli Ndg Ismail Abasi (Wa Pili Kulia) kujionea Ng'ombe wa maziwa aliowanunua kutokana na mafanikio ya mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe.Wengine ni Wataalamu wa utafiti kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa kilimo cha Kitropiki (IITA) Ndg Bakari Abdallah na Bi MaryJane Clemence
Mkulima wa zao la maharagwe Kitongoji cha Dukani, Kijiji na Kata ya Baga, Wilaya ya Bumbuli Ndg Ismail Abasi (Wa Pili Kulia) akielezea jinsi alivyonufaika na mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe.
Afisa Kilimo wa Kata ya Baga Wilayani Bumbuli Mkoani Tanga Ndg Elisafi Mashauri Mbaga akielezea jinsi wakulima wa maharagwe walivyonufaika na mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe.
Afisa Kilimo wa Kata ya Baga Wilayani Bumbuli Mkoani Tanga Ndg Elisafi Mashauri Mbaga (Kulia) akielezea jinsi wakulima wa maharagwe walivyonufaika na mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe.Wengine ni Wataalamu wa utafiti kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa kilimo cha Kitropiki (IITA) Ndg Bakari Abdallah na Bi MaryJane Clemence
Wataalamu wa utafiti kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa kilimo cha Kitropiki (IITA) wakiwa kazini Wilaya ya Bumbuli kuwatembelea wananchi kuona namna walivyonufaika na Mradi wa N2AFRICA
Athumani Ismail mtoto wa Mkulima wa zao la maharagwe Kitongoji cha Dukani, Kijiji na Kata ya Baga, Wilaya ya Bumbuli Ndg Ismail Abasi akielezea jinsi alivyonufaika na mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe kwa kulipiwa ada na hatimaye sasa kuelekea kujiunga na chuo kikuu.
Mkulima Ismail Abasi akionyesha jinsi alivyoboresha nyumba yake kutokana na mradi wa N2AFRICA katika kilimo cha maharagwe.

Na Mathias Canal, Tanga

Wakulima wadogo wameuomba mradi wa N2AFRICA unaojihusisha na usambazaji wa teknolojia ya mazao jamii ya mikunde hususani maharagwe kuwasaidia mbegu zingine ili kuongeza uzalishaji wa mazao mengi kwa manufaa kama ilivyo katika zao la awalila maharagwe walilopatiwa mbegu na elimu bora ya kilimo.

Mradi huo ambao upo chini ya Taasisi ya Kimataifa ya utafiti wa Kitropiki (IITA) umesaidia wakulima Wilayani Bumbuli Mkoani Tanga kupata elimu ya kilimo bora kupanda kwa kuacha nafasi, Kutumia mbegu bora na kulima maharagwe kwa kutumia mbolea tofauti na walivyokuwa wakilima kabla ya mradi huo.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima wengine wanufaika wa mradi huo Ndg Ismail Abasi aliomba kuongezwa mbegu nyingi za kilimo jamii ya mikunde ambazo ni pamoja na maharagwe yenyewe, kunde, mbaazi, karanga, soya, na choroko kwani ni mazao ambayo yanastawi kwa wingi katika maeneo hayo ya baridi.

Alisema katika nchi mbalimbali Barani Afrika ikiwemo Tanzania, upotevu wa mazao mashambani ni karibu asilimia 25 Kati ya mavuno yaliyotarajiwa kuvunwa hupotea huku robo tatu ya mavuno yote ambayo hupatikana salama.

Alisema hiyo robo tatu ya mavuno,  nayo hubaki ikiwa shakani kutokana na wadudu waharibifu na kuhifadhiwa katika maghala ambayo yapo chini ya kiwango.  

Alisema japo mradi huo wa N2AFRICA umewasaidia wakulima kulima kitaalamu lakini wanapaswa kuongeza ufanisi kwa kutoa viuatilifu kwa ajili ya kuuwa wadudu shambani kwani vilivyopo vinauzwa gharama kubwa ambazo sio rahisi wakulima wote kuzimudu.

Aliongeza kuwa Baadhi ya mazao, kama vile matunda, mboga za majani na mazao ya mizizi yanapotea mashambani kwa  asilimia 50,  ikiwa ni  mavuno yote ambayo yalitarajiwa kuvunwa hivyo ni hatari kwa mkulima kutokana na nguvu nyingi anazowekeza shambani lakini mavuno yanakuwa kidogo.

Akizungumzia jinsi wakulima walivyonufaika na mradi huo tangu ulipoingia Wilayani Bumbuli Afisa Kilimo wa Kata ya Baga Wilayani Bumbuli Mkoani Tanga Ndg Elisafi Mashauri Mbaga alisema tangu wakulima walipopatia mafunzo ya namna ya kuboresha kilimo chao ikiwemo kutumia mbegu na mbolea bora wamebadilisha maisha yao kwa kiasi kikubwa.

Alisema kuwa wapo waliofanikiwa kwa kuwalipia ada watoto wao, kufanya marekebisho ya nyumba zao, kununua bodaboda, kuboresha mazingira ya ndani ya nyumba na kuwa na kipato cha kukidhi mahitaji muhimu ya binadamu.

Alisema pamoja na mambo mengine yupo adui mkubwa kwenye zao la maharagwe kwa wananchi katika vijiji mbalimbali Katika Kata hiyo ikiwa ni pamoja na madoa pembe, na kutu.

Hata hivyo alisema kuwa magonjwa yanayo sababishwa na bakteria na virusi punguza magonjwa hayo ni kupanda mbegu safi, aina zinazo vumilia na kutunza shamba na unaweza kutumia madawa kama kocide, fugulani, Bayleton  kwa kuzuia magonjwa yanayosababishwa na ukungu na bakteria.

Mradi wa N2AFRICA unaendeshwa na na Taasisi ya Kimataifa ya kilimo cha Kitropiki katika ukanda wa joto makao makuu yake ni nchini Nigeria chini ya ufadhili wa Bill na Melinda Gates na kuongozwa na Chuo Kikuu cha Wagenigen cha Uholanzi.

MWISHO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com