METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, August 30, 2017

RPC SHANNA-AWAKALIA KOONI WAZAZI WALIOKATISHA MASOMO WATOTO WAO

SAM_5288
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

KAMANDA wa polisi mkoani Pwani,(ACP),Jonathan Shanna ametoa wiki moja kwa wazazi na walezi wanaowanyima watoto wao haki ya elimu kwa kuwaingiza katika ndoa za utotoni na wengine kutumikishwa kazi za kijamii kuwapeleka shule kabla hawajachukuliwa hatua.

Amesema kutokana mambo hayo atakuwa mkali na wanatarajia kuanza operesheni ya kuwafichua wazazi wanaokatisha masomo watoto .

Aidha amesema jeshi la polisi mkoani hapo limekamata silaha tatu katika wilaya ya kipolisi Mlandizi,Kibaha na Bagamoyo, ikiwemo shortgun isiyokuwa na namba ikiwa imekatwa mtutu,RIFLE MARK na shortgun yenye namba 68687.

Akizungumza wakati akikagua gwaride maalum kwa askari mjini Kibaha,kamanda Shanna alieleza,haikubaliki/haiwezekani kuwa na mkoa wenye lundo la watoto wasio na elimu.

Alisema watashirikiana na watendaji wa vitongoji,kata na maafisa elimu ili kuhakikisha elimu kwa watoto ipewa kipaumbele kuendana na kasi ya rais dk.John Magufuli.  

Alisema watakwenda nyumba kwa nyumba,shamba kwa shamba kuwafichua watoto waliofichwa na watawachukulia hatua wazazi ambao watakiuka agizo hilo.

“Nitakuwa mkali zaidi ya pilipili,”watoto wote walioachishwa shule warudi shuleni mara moja,na wazazi walioshiriki kuozesha watoto watachukuliwa hatua a kisheria ambao haijawahi kutokea duniani.”

“Kuna tabia ya watu kuhamia mashambani tutawafuata mashambani,tutakwenda hadi huko,askari wangu wana molari,wapo vizuri hadi Pwani itakapokuwa shwari kwa mikakati yake”alisema .

Hata hivyo kamanda Shanna alisema pia wanapambana na madawa ya kulevya na kufanikiwa kukamata bangi kg moja na heroin gram 1.20.

Alisema pia huko wilaya ya kipolisi Chalinze ilifanyika operesheni na kufanikiwa kukamata mitambo miwili ya kutengeneza pombe ya moshi .

Kamanda huyo,alieleza,wanaendelea na misako na doria mbalimbali katika maeneo ya mkoa wa Pwani,kuhakikisha wanatokomeza uhalifu kwa kiasi kikubwa .

Kamanda Shanna ,alitoa rai kwa wananchi kwa ujumla kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kuwafichua wahalifu waliopo kwenye maeneo yao ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema kwa kufuata mikakati waliojiwekea ikiwa ni sanjali na operesheni ya kuwafichua watoto waliokatishwa masomo yao na kupunguza uhalifu anaamini watafanikiwa kutokomeza changamoto hizo na uhalifu mkoani hapo .

Baadhi ya wananchi wilayani Kibaha,akiwemo Amina Shaha na Jumanne Anas walisema kufanyika kwa operesheni hiyo ya kuhakikisha watoto waliokatishwa masomo wanapelekwa shule ni jambo jema .

Anas alisema jukumu la wazazi ni kuwainua watoto wao katika suala zima la kuwapa elimu .
Amina alieleza,wapo baadhi ya wazazi ambao wanawatumikisha watoto wao kuuza biashara za familia kama karanga,mbogamboga na wengine kuwaozesha wakiwa wadogo.
Alisema tabia hiyo ikomeshwe ili iwe fundisho kwa wazazi wenye tabia hizo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com