Kampuni ya Huduma za Simu nchini ya Tigo leo imeamua kumuunga mkono Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe Dkt Angeline Mabula kwa kumkabidhi madawati Mia Moja kwa lengo la kupunguza changamoto za utoaji wa Elimu ili kuimarisha sekta hiyo Jimboni humo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yao kwake
Akizungumza wakati wa upokeaji wa madawati hayo Mhe Dkt Angeline Mabula mbali na kuishukuru Kampuni ya Tigo kwa namna inavyojitoa katika kusaidia huduma mbalimbali za kijamii amesema kuwa Tigo imekuwa kampuni inayowajibika kwa kutekeleza ahadi zake inazozitoa
‘… Kwakweli tunawashukuru wenzetu wa Tigo wamekuwa wakitekeleza kile inachokiahidi na tumekuwa na mahusiano nao mazuri na ninaimani tutaendelea kusaidiana, Tigo ni watu wasikivu wakiahidi wanatoa na wakisema hawana basi inakuwa ni kweli hawana …’ Alisema
Aidha Kampuni hiyo ya Tigo imepanga kusambaza Simu za Mezani kwa Shule za Jimbo la Ilemela lengo likiwa ni kurahisisha Mawasiliano ndani ya Jimbo hilo
Kwa upande wake Meneja wa Tigo Mkoa wa Mwanza Ndugu Kassim Aziz amesema kuwa huu ni muendelezo wa Kampuni yake katika kuunga mkono Serikali na Mbunge wa Jimbo la Ilemela kuhakikisha yanakuwepo mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia sanjari na kupunguza changamoto zinazoikabili Sekta ya Elimu
Makabidhiano hayo yalihusisha pia Viongozi wa Manispaa ya Ilemela akiwemo Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mhe Renatus Mulunga na Mkurugenzi wake John Wanga wakiwa na Kamati ya Fedha ya Manispaa hiyo
‘ Ilemela ni yetu, tushirikiane kuijenga ’
Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ilemela
30.08.2017
0 comments:
Post a Comment