Mtoto wa kike aliyezaliwa na ulemavu
sehemu ya uso amefariki dunia baada ya mama yake kugoma kumnyonyesha maziwa.
Mtoto huyo alizaliwa jumapili Agost
27 bila macho na pua ikiwa juu ya paji la uso. Kwa mujibu wa familia, mama wa
mtoto huyo Mariam Mwakombo (22) aligoma kumnyonyesha kwani alikuwa akiogopa.
“Mtoto nilijifungua usiku na alikuwa
akilia sana ila niliogopa kumshika kwani alikuwa na maajabu” aliliambia gazeti
la Kenya Nation.
Mwakombo alihudhuria mara mbili
kliniki ya kijiji cha Kilifi kwa muda wote mpaka kujifungua na wanakijiji
walipanga kumtupa mtoto huyo lakini baada ya kufariki dunia walimzika nje ya
nyumba ya familia.
Source: Kenya Nation Newspaper.
0 comments:
Post a Comment