Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi
na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu (katikati) akisisitiza jambo wakati
wa kikao cha Utendaji Kazi kati ya Menejimenti ya Wakala, Mameneja wa
Mikoa na Wakuu wa Vituo kilichofanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko
jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Ukodishaji Mitambo na
Huduma za Vivuko Mhandisi Japhet Y. Maselle na kushoto ni Jonas Bakuza,
Kaimu Mhasibu Mkuu wa wakala huo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi
na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu (katikati) akisisitiza jambo wakati
wa kikao cha Utendaji Kazi kati ya Menejimenti ya Wakala, Mameneja wa
Mikoa na Wakuu wa Vituo kilichofanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko
jijini Dar es Salaam. Wa kwanza Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji
Hans G. Lyimo, Mkurugenzi wa Ukodishaji Mitambo na Huduma za Vivuko
Mhandisi Japhet Y. Maselle. Kushoto kwa Dkt. Mgwatu ni Kaimu Mhasibu
Mkuu wa wakala huo Jonas Bakuza na Mkurugenzi wa Uzalishaji na
Matengenezo Mhandisi Sylvester Simfukwe. Kikao hicho kilijadili
Maandalizi na utekelezaji wa bajeti za Mikoa na Vituo, mabadiliko ya
sheria mbalimbali pamoja na Taratibu za Ununuzi.
Ndugu Hans G. Lyimo, Kaimu
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) akitoa
ufafanuzi wakati wa Kikao cha Utendaji Kazi Kati ya Menejimenti ya
Wakala, Mameneja wa Mikoa na Wakuu wa Vituo kilichofanyika katika ukumbi
wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam. Wa pili Kulia ni Mkurugenzi wa
Ukodishaji Mitambo na Huduma za Vivuko Mhandisi Japheth Y. Maselle,
Mtendaji Mkuu wa wakala huo Dk. Mussa Mgwatu, Kaimu Mhasibu Mkuu Jonas
Bakuza na Mkurugenzi wa Uzalishaji na Matengenezo Mhandisi Sylvester
Simfukwe. Kikao hicho kilijadili Maandalizi na utekelezaji wa bajeti za
Mikoa na Vituo, mabadiliko ya sheria mbalimbali pamoja na Taratibu za
Ununuzi.
Meneja wa Wakala wa Ufundi na
Umeme (TEMESA) Mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi Alfred Ng’wani akitoa hoja
wakati wa kikao cha Utendaji Kazi kati ya Menejimenti ya Wakala,
Mameneja wa Mikoa na Wakuu wa Vituo kilichofanyika katika ukumbi wa Mt.
Depot Keko jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kilijadili Maandalizi na
utekelezaji wa bajeti za Mikoa na Vituo, mabadiliko ya sheria mbalimbali
pamoja na Taratibu za Ununuzi.
0 comments:
Post a Comment