Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Tanzania Girl Guides
(TGGA), Anna Abdallah (katikati) akiwa na Girl Guides waliorejea nchini
kutoka kwenye programu ya Yess ya kubadilishana uzoefu katika masuala ya
uongozi, utamaduni na maadili katika nchi za Uganda, Madagascar,
Zimbabwe na Zambia. Hapo ilikuwa wakati wa hafla maalumu iliyoandaliwa
na TGGA Dar es Salaam kwa ajili ya kuwapongeza na kupata mrejesho wa
walichojifunza walipokuwa kwenye programu hiyo inayodhaminiwa na
Norwey.Anna Abdallah aliwapongeza wasichana hao wanne kwa kuiwakilisha
vizuri TGGA na Tanzania katika programu hiyo nje ya nchi.
Kutoka kulia ni Ummy Mwabondo alikwenda Zambia, Farida Mjoge aliyekuwa Uganda, Elizabeth Betha (Madagascar) na Edna Chembele (Zimbabwe),
Girl Guides hao wakipata msosi wakati wahafla ya chakula cha usiku
iliyoandaliwa kwa ajili yao kwenye Hoteli ya Golden Tulip, Oysterbay,
Dar es Salaam.
Anna Abdallah akiotoa nasaha na pongezi kwa Girl Guides kwa
kuiwakilisha vizuri TGGA NA Tganzania kwa ujumla, ambapo aliwataka
watumie mafunzo waliyoyapata kwa kutoa mafunzo kwa wasichana wenzao
nchini.
Wakiwa na furahani Kamishna Mkuu wa TGGA, Symphorosa Hangi (kushoto), Anna Abdallah (katikati) na Mjumbe wa TGGA, Agnes Makenya
Katibu Mkuu wa TGGA Tanzania, Grace Shaba akitoa neno la ukaribisho
muda mfupi kabla ya Girl Guides waliorejea nchini kutoka nje ya nchi
kwenye programu hiyo kuelezea mambo mbalimbali waliyoyafanya na
kujifunza
Grace Shaba akiwatambulisha Girl Guides hao
i Ummy Mwabondo akielezea kwa njia ya picha kazi mbalimbali alizokuwa anazifanya alipokuwa Zambia
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya TGGA, Sophia
Mjema akitoa ufafanuzi wakati Girl Guides wakielezea mafanikio na
changamoto ya mafunzo yao nje ya nchi
Girl Guides Farida akielezea mambo mbalimbali aliyoyafanya akiwa Uganda kwa muda wa miezi sita.
Monday, August 14, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
-
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe jana Tarehe 17 Juni 2019 aki...
-
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Mhandisi Mathew Mtigumwe anautangazia Umma kuwa, Wizara imeandaa Mkutano wa Wafanyabi...
-
HOTUBA YA KUTANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KATIKA JIMBO LA ISIMANI KWA TIKETI YA CHAMA CHA MAPINDUZI MWAKA 2015 UTANGULIZI UTA...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment