- Imeandikwa na Isdory Kitunda
- MKAZI wa Kijiji cha Nyarero, tarafa ya Inchage, wilayani Tarime,
mkoani Mara, Magita Enoshi (50) amehukumiwa kwenda jela maisha baada ya
kupatikana na hatia ya kushambulia kwa mapanga na kumkatakata jirani
yake, John Kichere sehemu mbalimbali za mwili na kumsababishia ulemavu
wa maisha.
Akisomewa hukumu hiyo mwishoni mwa wiki, Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza, Joaquine De-Mello alisema ameridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka ukiongozwa na mwanasheria wa Serikali, Harry Mbogoro.
Awali ilidaiwa kuwa mtuhumiwa Enoshi, mnamo Oktoba 20, mwaka 2010 saa moja jioni kwa nia mbaya ya chuki akiwa na panga alimshambulia Kichere ambaye ni jirani yake kwa kumkatakata mapanga sehemu mbalimbali za mwili zikiwemo mkono na kukatika vidole vitatu, kumkata shingoni na mgongoni na kumsababishia majeraha makubwa na kupoteza fahamu kwa muda.
Ilidaiwa kuwa baada ya kukimbizwa hospitali kupatiwa matibabu yaliyochukuwa muda mrefu kupata nafuu, sasa majeruhi amepata ulemavu wa kudumu. Awali mtuhumiwa huyo alikana shitaka hilo na upande wa utetezi wake ukiongozwa na wakili wa kijitegemea, Msafiri Henga alidai kuwa mlalamiko ya Kichere dhidi ya mteja wake, Enoshi yalikuwa ya chuki. Hata hivyo, kutokana na ushahidi, Jaji De-Mello alisema imedhihirisha kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo. “Ninakuhukumu kwenda jela maisha ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye nia mbovu ya kuwadhuru wenzao,” alisema Jaji De-Mello.
Tuesday, May 16, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa upinzani, Kizza Besigye akisindikizwa na maofisa wa gereza la Luzira alikokuwa akishikiliwa Kiongozi w...
-
Na Mathias Canal, WAZOHURU MEDIA Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali...
-
Mjumbe Halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi Taifa MNEC Salim Abri Asas akiongea na wananchi wa Mkoa wa Iringa wakati wa uzinduzi wa miaka...
-
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akikagua bwalo la chakula na madarasa, katika shule ya sekondari ya bweni ya Lucas Malia, iliyopo wilay...
-
Na Debora Charles (Mtakwimu) Sensa ya watu na makazi ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua, kutathimini na kuchapisha na kusamba...
Powered by Blogger.

0 comments:
Post a Comment