- Imeandikwa na Isdory Kitunda
- MKAZI wa Kijiji cha Nyarero, tarafa ya Inchage, wilayani Tarime,
mkoani Mara, Magita Enoshi (50) amehukumiwa kwenda jela maisha baada ya
kupatikana na hatia ya kushambulia kwa mapanga na kumkatakata jirani
yake, John Kichere sehemu mbalimbali za mwili na kumsababishia ulemavu
wa maisha.
Akisomewa hukumu hiyo mwishoni mwa wiki, Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza, Joaquine De-Mello alisema ameridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka ukiongozwa na mwanasheria wa Serikali, Harry Mbogoro.
Awali ilidaiwa kuwa mtuhumiwa Enoshi, mnamo Oktoba 20, mwaka 2010 saa moja jioni kwa nia mbaya ya chuki akiwa na panga alimshambulia Kichere ambaye ni jirani yake kwa kumkatakata mapanga sehemu mbalimbali za mwili zikiwemo mkono na kukatika vidole vitatu, kumkata shingoni na mgongoni na kumsababishia majeraha makubwa na kupoteza fahamu kwa muda.
Ilidaiwa kuwa baada ya kukimbizwa hospitali kupatiwa matibabu yaliyochukuwa muda mrefu kupata nafuu, sasa majeruhi amepata ulemavu wa kudumu. Awali mtuhumiwa huyo alikana shitaka hilo na upande wa utetezi wake ukiongozwa na wakili wa kijitegemea, Msafiri Henga alidai kuwa mlalamiko ya Kichere dhidi ya mteja wake, Enoshi yalikuwa ya chuki. Hata hivyo, kutokana na ushahidi, Jaji De-Mello alisema imedhihirisha kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo. “Ninakuhukumu kwenda jela maisha ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye nia mbovu ya kuwadhuru wenzao,” alisema Jaji De-Mello.
Tuesday, May 16, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa upinzani, Kizza Besigye akisindikizwa na maofisa wa gereza la Luzira alikokuwa akishikiliwa Kiongozi w...
-
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Mbunge wa Kisarawe Selemani Jafo akijiandaa kukata keki katika katika sherehe ya kuwapongeza...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya kilim...
-
Na Munir Shemweta, WANMM Serengeti Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula ameagiza zoezi...
-
Kuangalia video za ngono sio jambo jipya kwa jamii yetu, kimsingi ni watu wachache sana wanaweza kujizuia kujichua au kupiga punyeto ...
Powered by Blogger.

0 comments:
Post a Comment