METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, March 16, 2017

Shirika la Mazingira la Umoja wa mataifa laipongeza Kenya kupiga marufuku mifuko ya plastiki



Shirika la mipango ya mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP limeipongeza Kenya kwa kupiga marufuku uzalishaji, uagizaji na matumizi ya mifuko ya plastiki.

Mkurugenzi mtendaji wa UNEP Bw Erik Solheim amesema hatua hiyo itaanza kutekelezwa mwezi Agosti na inatarajiwa kuhimiza wengine kuunga mkono kampeni ya kuwa na bahari safi.

Waziri wa mazingira na maliasili wa Kenya Bibi Judy Wakhungu ametangaza amri hiyo ya serikali ambayo itaanza kutekelezwa ndani ya miezi sita. Tangazo hilo limetolewa wakati Kenya inatumia mifuko ya plastiki ipatayo milioni 100 kila siku, na kuleta changamoto kubwa kwenye uondoaji wa taka za plastiki.

Wiki tatu zilizopita UNEP ilitangaza vita dhidi ya matumizi ya plastiki, kupitia mpango wake wa kusafisha bahari, na kusema serikali kumi zimeunga mkono mpango huo.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com