
Kamati ya Utalii ya Halmashauri ya Jiji
la Mbeya ikiongozwa na Afisa Utalii wa Jiji Bi.Levina Modest na
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.Geofrey Kajigili wanaofanya kampeni hii
kabambe ya utambuzi wa Vivutio vyote vilivyopo Jijini Mbeya kwa
kushirikiana na asasi zisizo za kiserikali za Uyole Cultural Tourism
Enterprise pamoja na Elimisha .
Pia wamemtembelea Mzee Mkongwe wa Siasa
nchini, Mzee Rashid Ally Sinkala ambaye amewahi kuwa Diwani wa iliyokuwa
ikiitwa Kata ya Soko Matola (sasa Kata ya Maendeleo) kwa miongo
kadhaa,na amewahi kutumika kama Meya ya Halmashauri ya Mbeya Mjini.
Mzee Sinkala ameiambia Kamati ya Utalii
kuwa Miaka zaidi ya 50 iliyopita wakati wa Siasa za Ukombozi wa
Tanganyika enzi za Chama cha Tanganyika African National Union
(TANU)Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa akifikia kwenye
nyumba ya mwanasiasa Mkongwe mwanamke aliyejulikana kwa majina ya
Zaituni Binti Matola.Binti Matola alitenga chumba kimoja nyumbani kwake
kama Maficho ya Mwalimu Nyerere.

Mzee Sinkala akiwa mlangoni mwa Chumba maalum alipokuwa akifikia Mwalimu Nyerere ndani ya nyumba ya muasisi wa TANU na mwanamke mashuhuri Hayati Zaituni Binti Matola aliyesababisha maeneo hayo kuitwa "Soko Matola" Jijini Mbeya

Wajumbe wa Kamati ya Utalii Jijini Mbeya
wakimsikiliza kwa makini Meya mstaafu wa Halmashauri ya Mbeya Mjini
Mzee Sinkala ndani ya nyumba ya kihistoria ya Binti Matola.
0 comments:
Post a Comment