METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, March 1, 2016

Waziri Nape kunogesha Tamasha la Pasaka

ri Nape kunogesha Tamasha la Pasaka

Waziri Nape 
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, anatarajia kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Pasaka litakalofanyika jijini Mwanza Machi 27.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama, kamati yake inaendelea na maandalizi ya kuelekea tamasha hilo ambalo litashirikisha waimbaji mbalimbali hapa nchini.
 
“Maandalizi kuelekea Tamasha la Pasaka yanaendelea vema, hivyo wakazi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa wajiandae kupokea ujumbe wa neno la Mungu kupitia viongozi wa dini na waimbaji wa muziki wa Injili,” alisema Msama.

Msama alisema baadhi ya waimbaji  wamethibitisha kushiriki tamasha hilo ambao ni pamoja na Rose Muhando, Bonny Mwaitege, Upendo Nkone, Jesca BM Honore, Christopher Mwahangila, Joshua Mlelwa, Sifael Mwabuka, Jenipher Mgendi, Kwaya ya AIC Makongoro na Kwaya ya Wakorintho Wapili.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com