HATIMAYE
Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli imekisikia kilio
cha muda mrefu cha Wananchi ambao walikuwa wakilalamika kupanda kwa
bei ya sukari nchini.
Akizungumza na Waandishi wa Habari
mchana huu jijini Dar es Salaam Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Sukari
nchini,Henry Semwaza amesema kuanzia sasa kilo moja ya sukari itauzwa
sh. 1800 nchi nzima.
"Serikali, kupitia bodi ya Sukari
Tanzania, inawaarifu wananchi wote kuwa bei ya rejareja ya sukari sasa
itakuwa sh. 1,800 kwa kilo moja. "Amesema Semwaza na kuongeza;
"
Wafanyabiashara wote wanapaswa kuzingatia agizo hili, pamoja na
kuhakikisha kuwa sukari inaendelea kusambazwa na kuuzwa kwa wananchi
bila kuihodhi.
"Maafisa biashara wa mikoa na wilaya watafuatilia
na kusimamia utekelezaji wa agizo kuhusu bei elekezi ya sukari, na
hawatasita kuchukua hatua stahiki za kisheria kwa wale watakaobainika
kupandisha bei ya bidhaa hiyo. "
Tuesday, March 8, 2016
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Nimebahatika kupata fursa kadhaa kukaa na kuzungumza na Mheshimiwa Rais Mstaafu Hayati Benjamin William Mkapa enzi za uhai wake....
-
Na Mathias Canal, WAZOHURU MEDIA Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali...
-
Na THEOFLIDA WA YESU Naanza kwa kuwasalimu kwa JINA LA YESU. Jina lililo Kuu kupita majina yote. Wiki ...
-
Mbunge wa Nzega Vijijini ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa pamoja na Mgombea nafasi ya Udi...
-
Kuangalia video za ngono sio jambo jipya kwa jamii yetu, kimsingi ni watu wachache sana wanaweza kujizuia kujichua au kupiga punyeto ...
Powered by Blogger.


0 comments:
Post a Comment