METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, June 8, 2015

MTOTO WA MUGABE APATIKANA NA HATIA

 
 
Mwana mkubwa wa kiume wa mke wa rais wa Zimbabwe Grace Mugabe amepatikana na hatia ya kuua bila kukusudia na kupigwa faini ya dola 800.
 
Russell Goreraza alimgonga na kumuua mwanamume mmoja ambaye hakutambuliwa katika gari lake katika mji mkuu wa Harare mnamo mwezi Februari.

''Ninajuta na ningependa kuomba msamaha kwa kitendo hicho'', Kijana huyo wa miaka 31 aliimbia mahakama.

Hakimu huyo alisema kuwa aliamua kuifutilia mbali leseni ya kijana huyo na kumpatia hukumu ya kifungo cha jela lakini akabadilisha nia yake kutokana na majuto yake.

Douglas Chikwekwe amesema kuwa hatua kwamba Goreraza alitekeleza kitendo hicho kwa mara ya kwanza pia kuliathiri uamuzi wake.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com