METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, May 15, 2023

MBUNGE NJEZA AMETAKA KUJUA JE NI LINI SERIKALI ITAJENGA BARABARA YA MCHEPUKO YA MLIMA NYOKA(UYOLE) HADI UWANJA WA NDEGE WA SONGWE ILI KUONDOA MSONGAMANO NA AJALI


Na Saida Issa, Dodoma

SERIKALI imesema kuwa ipo kwenye maandalizi ya kujenga barabara ya Igawa  Songwe  Tunduru (km 218) pamoja na barabara ya mchepuo ya Mlima wa Nyoka (Uyole) hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe (Uyole  Songwe Bypass) yenye urefu wa kilometa 48.9 kwa utaratibu wa EPC+F (Engineering, Procurement, Construction plus Finance). 

Hayo ameyaeleza Naibu Waziri Ujenzi na uchukuzi Mhandisi Geodfref Kasekenya alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mbeya Vijijini Oran Manase Njeza, alipouliza Je, ni lini Serikai itajenga barabara ya Mchepuko ya Mlima Nyoka (Uyole) hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe ili kuondoa msongamano na ajali.

Naibu Waziri huyo amesema kuwa Hadi sasa Mkandarasi ameshapatikana na mkataba wa ujenzi utakuwa umesainiwa kabla ya mwisho wa Mwezi Juni, 2023.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com