

Mwenyekiti wa
umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi Taifa (UVCCM) Ndg.Mohamed Ali Kawaida akiwa katika picha ya pamoja na makamu Mwenyekiti (UVCCM) Taifa Ndg. Rehema Sombi na katibu mkuu (UVCCM) Taifa Ndg. Kenan Kihongosi
katika hafla ya mapokezi ya viongozi wakuu wa umoja wa vijana wa chama cha
mapinduzi Taifa (UVCCM) mkoani singida 18 Disemba 2022.
Na Rasuli
Kidindi, Juma Wage Singida.
Mwenyekiti wa
umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi Taifa (UVCCM) Ndg.Mohamed Ali Kawaida amewaonya wanaobeza ziara zinazofanywa na Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan nje ya nchi huku
akisema ziara hizo ni zakutafuta fursa mbalimbali ikiwemo uwekezaji na sio za
kutembea.
Ndg.
Mohamedi Ali kawaida ameyasema hayo Disemba 18 mkoani Singida katika hafla ya
mapokezi ya viongozi wakuu wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi Taifa (UVCCM) mkoani humo akiwa ameongozana na makamu mwenyeki (UVCCM) Taifa Ndg. Rehema
Sombi na katibu mkuu (UVCCM) Taifa Ndg. Kenan Kihongosi ambapo amesema jumuiya
hiyo haitawavumilia wanaobeza ziara mbalimbali za Rais Dkt. Samia Suluhu
Hassan.
Aidha Ndg.
Mohamed Ali Kawaida amesema wataendeleza na kuulinda umoja wa vijana kwa
manufaa ya chama pamoja na maendeleo ya nchi.
“ Umoja wetu
wa vijana tutauendeleza na kuulinda na yoyote atakayezingua tutamchapa” alisema
Kawaida
Kwa upande
wake makamu Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi Taifa (UVCCM) Ndg.
Rehema Sombi ameahidi kufanya kazi kwa waledi na kujituma ili kuwalipa imani vijana kwa kuwaamini na kuwachagua kuwa viongozi wao huku akisisitiza uchaguzi
umekwisha sasa ni muda wa kufanya kazi na kuacha makundi.
Pia Ndg.
Rehema Sombi ametumia fursa hiyo kuwaasa vijana kujiepiusha na matumizi ya madawa ya kulevya pamoja na kutumia vizuri mitandao ya kijamii.
Awali naye katibu
mkuu wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi Taifa (UVCCM) Ndg. Kenan Kihongosi akatumia fursa hiyo kuwataka
vijana kuacha chuki, fitna na majungu na kujikita katika kufanya kazi .
Pamoja na
mambo mengine vilevile Ndg. Kenan Kihongosi amewasihi vijana kukilinda chama
na kuyasemea mambo mazuri yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa
na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
0 comments:
Post a Comment