METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, August 12, 2020

KATIBU MKUU KILIMO AWAPONGEZA VIONGOZI WA KIWANDA CHA KAGERA SUKARI KWA KUANZA MRADI WA KUONGEZA UZALISHAJI MKUBWA WA SUKARI

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha sukari cha Kagera Bwana Ashwin Rana mapema leo tarehe 12 Agosti, 2020 wakati wa ziara yake ya kutembelea shughuli za maendeleo ya Sekta ya Kilimo wilayani Missenyi, mkoani Kagera

KatibuMkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya pamoja na ujumbe wake wakimsikiliza Nestory Rwechungura, Mhandisi Mkuu wa mitambo ya kiwanda cha sukari cha Kagera, mapema leo tarehe 12 Agosti, 2020 wakati wa ziara yake ya kutembelea shughuli za maendeleo ya Sekta ya Kilimo wilayani Missenyi, mkoani Kagera

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya, Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha sukari cha Kagera Bwana Ashwin Rana pamoja na Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Sukari na ujumbe ulioambatana nao kutoka Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Kagera mapema leo tarehe 12 Agosti, 2020 wakati wa ziara yake ya kutembelea shughuli za maendeleo ya Sekta ya Kilimo wilayani Missenyi, mkoani Kagera.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya mapema leo tarehe 12 Agosti, 2020 amewapongeza Viongozi na Wafanyakazi wa kiwanda cha sukari Kagera kwa kutanguliza maslai ya taifa mbele kwa kuongeza eneo la kilimo cha miwa kiasi cha hekta elfu 16 (16,000) ambapo uzalishaji unatarajiwa kufika kiasi cha tani 170,000.

Katibu Mkuu amesema hatua hiyo ni ya kujivunia kama nchi kwa kuwa Taifa limekuwa likipitia changamoto ya kukosa sukari katika kipindi cha mwezi Machi hadi Mei kila mwaka; kutokana na viwanda vyote vinne vinavyozalisha sukari nchini kusimamisha uzalishaji kwa kuwa huo si wakati mzuri wa kilimo cha miwa kutokana sababu ya mvua za masika.

Katibu Mkuu ameongeza kuwa mahitaji ya sukari nchini kiasi cha tani 470,000 wakati uzalishaji wetu ufikia tani 359,000.

“Nawapongeza kiwanda cha Kagera sukari kwani baada ya uapnuzi wa kiwanda pamoja na kuongezeka kwa eneo la kilimo la hekta 16,000 kuanzia mwaka 2024/25 taifa litapata ziada ya tani 170,000.” Amekaririwa Katibu Mkuu Kusaya.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com