METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, July 25, 2020

TAWA YAENDESHA KIKAO KAZI CHA UJIRANI MWEMA

IMG-20200725-WA0029.jpg
Baadhi ya  wadau wa  Utalii wakiwa katika kikao kazi cha kupitia mkakati wa  huduma za ujirani mwema  wa uhifadhi Kilichoandaliwa na Mamlaka ya usimamizi wa wanayamapori Tanzania  TAWA.
IMG-20200725-WA0038.jpg
 Wajumbe wa kikao kazi cha kupitia mkakati wa  huduma za ujirani mwema  wa uhifadhi Kilichoandaliwa na Mamlaka ya usimamizi wa wanayamapori Tanzania  TAWA kilichofanyika Mjini Morogoro
IMG-20200725-WA0045.jpg
PICHA ya pamoja ya wadau wa  Utalii wakiwa katika kikao kazi cha kupitia mkakati wa  huduma za ujirani mwema  wa uhifadhi Kilichoandaliwa na Mamlaka ya usimamizi wa wanayamapori Tanzania  TAWA mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho kilichofanyika Kingolwira Mkoani Morogoro makao makuu ya TAWA

MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA  imekutana na wadau mbalimbali wa  Utalii katika kikao kazi cha kupitia mkakati wa  huduma za ujirani mwema  wa uhifadhi kilichofanyika katika makao makuu ya mamlaka hiyo Kingolwira Mjini Morogoro
Kikao kazi hicho kimehusisha wadau mbalimbali wa uhifadhi kama vile halmashauri za Wilaya,wadau wa maendeleo,mashirika ya uhifadhi,vyuo  na watoa huduma za utalii
Akifungua Kikao kazi hicho cha siku Moja Kilichofanyika Leo July 25, 2020 Kamishna Mhifadhi wa TAWA  Mabula Misungwi  amewaomba wadau hao wa uhifadhi kushirikiana katika kuhifadhi kwa kuwalinda wanyamapori kwa maslahi ya Taifa.
Aidha Misungwi amesema kuwa TAWA imekuwa ikichangia miradi mingi ya kimaendeleo kwa jamii inayozunguka maeneo yanayohifadhiwa na mamlaka hiyo kupitia utalii wa picha na uwindaji wa kitalii.
Sanjari na hayo amesisitiza haja ya kuweka mpango wa kushirikiana katika kudhibiti wanyamapori waharibifu
Nae Bi Gloria Bideberi msimamizi wa kitengo cha Ujirani mwema  amesema kuwa fedha zilizotumwa na wadau wa utalii kwa kipindi cha mwaka 2017-2020 ni shilingi bilioni 4 fedha za kitanzania zilizotumika katika maendeleo ya jamii.
Kwa upande changamoto amesema kuwa WMA Inakabiliwa na uhaba wa vitendea kazi kama vile magari na sarae za askari wa vijiji
Nao baadhi ya wadau wa TAWA wameitaka mamlaka  hiyo kushirikiana katika kukabiliana na wanyamapori waharibifu wa mazao pia kusaidia vitendea kazi vya WMA kama vile mavazi na magari.
Mamlaka ya Usimamizi wa wanyamapori Tanzania TAWA  imendelea kuwa  mstari wa mbele katika Kuhakikisha jamii inanufaika na uhifadhi kwa  maeneo wanayowazunguka kwa kusaidia miradi ya maendeleo ikiwemo,afya elimu pamoja huduma ya maji safi na salama.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com