METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, July 29, 2020

RAIS MHE. DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AONGOZA WATANZANIA KATIKA MAZISHI YA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA TATU BENJAMIN WILLIAM MKAPA LUPASO MASASI MKOANI MTWARA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiweka udongo kwenye kaburi la Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa katika Mazishi yaliyofanyika katika Kijiji cha Lupaso Masasi Mkoani Mtwara.
Wanajeshi wa JWTZ wakiwa wamebeba Jeneza lenye Mwili wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa kuelekea eneo la Makaburi kwa ajili ya Mazishi yaliyofanyika katika Kijiji cha Lupaso Masasi Mkoani Mtwara
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Viongozi mbalimbali pamoja Wananchi wa Lupaso waliohudhuria katika Mazishi hayo ya Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa Lupaso Masasi mkoani Mtwara.
Mabregedia Jenerali wa JWTZ wakishuhudia Jeneza lenye Mwili wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa likishushwa kaburini Lupaso Masasi mkoani Mtwara.
Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia Mjane wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa Mama Anna Mkapa akiweka udongo kwenye kaburi la Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa katika Mazishi yaliyofanyika katika Kijiji cha Lupaso Masasi Mkoani Mtwara. PICHA NA IKULU.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com