METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, November 24, 2019

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Afunga Maonesho ya Wajasiriamali, katika Kusherehekea Miaka 20 ya Uanzishwaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, kwenye viwanja vya Fumba Zanziba


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Ali Abeid Karume, wakati akiwasili Mwenyekiti Viwanja vya Fumba, kufunga Maonesho ya Wajasiriamali, katika Kusherehekea Miaka 20 ya Uanzishwaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, Novemba 24, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea zawadi ya gazeti, kutoka kwa Mhariri Mtendaji wa Shirika la Magazeti ya Serikali Zanzibar, Yussuf Khamis, wakati akitembelea mabanda, kwenye Maonesho ya Wajasiriamali, katika Kusherehekea Miaka 20 ya Uanzishwaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, yaliyofungwa rasmi Novemba 24, 2019. Kutoka kushoto ni Maafisa Biashara na Matangazo, Rahma Juma,Khalid Hussein na Khadija Khamis.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifafanuliwa jambo na Afisa Manunuzi wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar, Shinuna Ismail, wakati akitembelea mabanda, kwenye Maonesho ya Wajasiriamali, katika Kusherehekea Miaka 20 ya Uanzishwaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, yaliyofungwa rasmi Novemba 24, 2019. Kutoka kushoto ni Maafisa Biashara na Matangazo, Rahma Juma,Khalid Hussein na Khadija Khamis.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa ameshika mwani, wakati akifafanuliwa jambo na Naibu Mkurugenzi Mkuu TAN TRADE, Latifa Khamis, kwenye Maonesho ya Wajasiriamali, katika Kusherehekea Miaka 20 ya Uanzishwaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, yaliyofungwa rasmi Novemba 24, 2019, kwenye viwanja vya Fumba Zanzibar.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwahutubia wananchi, kwenye Maonesho ya Wajasiriamali, katika Kusherehekea Miaka 20 ya Uanzishwaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, aliyoyafungwa rasmi Novemba 24, 2019
Wananchi waliofika Mwenyekiti ufungaji wa Maonesho ya Wajasiriamali, katika Kusherehekea Miaka 20 ya Uanzishwaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wakati akiwahutubia, kwenye Maonesho hayo, Novemba 24, 2019
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Mwenyekiti wa Wajasiriamali Jumuiya Afrika Mashariki, Josephat Royemam, kwenye Maonesho ya Wajasiriamali, katika Kusherehekea Miaka 20 ya Uanzishwaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, aliyoyafungwa rasmi Novemba 24, 2019. Kutoka Kushoto ni Waziri wa Biashara na Viwanda wa Zanzibar Balozi Amina Salum Ally na Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Shadya Mohamed. 

(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


 
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com