METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, September 26, 2019

MAJALIWA ATEMBELEA KIWANDA CHA NGUZO ZA UMEME CHA QWIHAYA MJINI MAFINGA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua nguzo za umeme zilizorundikana kwenye kiwanda cha Qwihaya General Enterprises Company LTD cha Mafinga zikisubiri wanunuzi. Kiwanda hicho cha nguzo kilitembelewa na Waziri Mkuu, Septemba 26, 2019. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda hicho, Leonard Mahenda, wa tatu kushoto ni Meneja Uzalishaji wa kiwanda hicho, Fred Ngwega na wa nne kusho ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Happy.
Nguzo za umeme zikiwa kwenye mtambo wa kuziwekea dawa maalum ya kuzifanya zisishambuliwe na wadudu au kuungua moto zikiwa katika kiwanda cha Qwihaya General Enterprises Company Limited cha mjini Mafinga ambacho kilitembelewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, September 26, 2019
Baadhi ya nguzo za umeme zilizorundikana zikisubiri wanunuzi kwenye kiwanda cha Qwihaya General Enterprises Limited cha mjini Mafinga ambacho kilitembelewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Septemba 26, 2019. {Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com