METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, June 6, 2019

Hii Ndiyo Miradi ya kimkakati Mwanza "Magari Yanapaki Chini ya Ardhi"

Halmashauri ya Jiji la Mwanza inatarajia kuanza utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ambayo ni pamoja na ujenzi wa soko kuu, stendi ya mabasi Nyegesi pamoja na kituo cha maegesho ya magari makubwa Buhongwa ambapo miradi hiyo itaongeza ukusanyaji wa mapato ya halmashauri hiyo.

Hayo yalisemwa jana Juni 05, 2019 na Mkurugenzi wa Jiji hilo, Kiomoni Kibamba wakati akizungumza kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika eneo la Soko Kuu.

"Kutakuwa na "parking" ya magari zaidi ya 500 kwa wakati mmoja chini ya ardhi...ukiingia na hela unatumbukiza kwenye mashine, inakupa chenchi..." alisema Kibamba.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com