METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, June 2, 2019

ANTHONY JOSHUA ACHAKAZWA MAREKANI, APIGWA KWA KO NA RUIZ

Bondia Muingereza Anthony Joshua akiwa chini baada ya kuangushwa na mpinzani wake, Mmarekani mwenye asili ya Mexico, Andy Ruiz Jr Alfajiri ya leo ukumbi Madison Square Garden mjini New York kwenye pambano la uzito wa juu. Joshua amevuliwa ubingwa wa dunia wa uzito wa juu duniani baada ya kupigwa kwa Technical Knockout (TKO) raundi ya saba. Ruiz hajawahi kuangushwa kabla, lakini naye leo alikalishwa chini raundi ya tatu, kabla ya kuinuka na kuendelea.
Joshua mwenye urefu wa futi sita atajaribu kurejesha mataji yake ya IBF, WBA na WBO katika pambano la marudiano Novemba. Hilo ni pambano la kwanza Joshua kupoteza baada ya kushinda mapambano yake yote 22 ya awali, 21 kwa knockout, wakati Ruiz mwenye urefu wa futi nne ameshinda pambalo la 32 na 22 kwa KO, huku akiwa amepoteza pambano moja pia 
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com