METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, January 14, 2018

SHAKA AMFAGILIA JAFO NA KUNIKUNI KISARAWE

   Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi(CCM) Shaka Hamdu Shaka  akiwa na Mbunge wa Kisarawe Selemani Jafo katika ufungaji wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kurui.
   Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi(CCM) Shaka Hamdu Shaka  akivishwa skafu wakati alipofika katika kata ya Kurui kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata hiyo.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi(CCM) Shaka Hamdu Shaka  akimnadi mgombea wa udiwani wa kata ya Kurui Mussa Kunikuni
  Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi(CCM) Shaka Hamdu Shaka  akipokea mmoja wa wanachama kutoka vyama vya upinzani
 Mbunge wa Kisarawe Selemani Jafo akizungumza katika ufungaji wa kampeni za udiwani kata ya Kurui
..................................................................................................
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi(CCM) Shaka Hamdu Shaka  amemwagia sifa Mbunge wa Jimbo la Kisarawe Mhe. Selemani Jafo kwa uchapakazi wake uliotukuka na hivyo amewataka wananchi wa kata ya Kurui wilayani Kisarawe wasifanye makosa kabisa wahakikishe wanamchagua Mussa Kunikuni kuwa diwani wa kata hiyo katika uchaguzi utakaofanyika kesho Januari 13, mwaka huu.

Akifunga kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wa Kata ya Kurui Shaka amesema wananchi watakapomchagua Mussa Kunikuni hapo kesho itasaidia kuleta maendeleo makubwa katika kata hiyo kwa kuwa atakuwa anaunganisha juhudi kubwa inayofanywa na Rais John Pombe Magufuli pamoja na Mbunge Jafo katika suala zima la utekelezaji wa Ilani ya CCM ndani ya kata hiyo na wilaya nzima kwa ujumla.


Naye,Mwenyeki wa mkoa wa Pwani ndugu Ramadhani Maneno amewataka wananchi wa kata hiyo kutofanya makosa katika uchaguzi wa kesho kwani mkoa mzima wa Pwani umeelekeza jicho lake katika kata hiyo ile kuleta heshima kwa mkoa wa Pwani.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com