METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, December 28, 2017

WAZIRI MWIGULU AWATAKA WANANCHI MTWARA KUJIANDIKISHA KWA AJILI YA KITAMBULISHO CHA TAIFA

Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Dr Mwigulu Nchemba amewataka kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Mtwara kushirikiana wote kwa pamoja katika zoezi la uandikishaji wa kitambulisho cha uraia ili pasiwepo na ambao si Raia wa Tanzania kuandikishwa kama Raia.

Waziri Dr Nchemba amewataka Watanzania hasa maeneo ya mipakani kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kujiandikisha kwa ajili ya vitambulisho vya uraia na kuwafichua wale ambao si Raia wa Tanzania ambao wamejitokeza sasa kuandikishwa ili pasiwepo baadae kesi za wasio watanzania kuandikishwa.

"Wananchi jitokezeni mtimize jukumu lenu la kujiandikisha hamnunui kitambulisho ni kutoa taarifa sahihi na zikikidhi mtapewa vitambulisho" Waziri Nchemba

Naye mkuu wa mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amesema kuwa zoezi la uandikishaji wa  kitambulisho cha taifa unaendelea vizuri changamoto kubwa wanayokutana nayo ni mwitikio mdogo wa wananchi kujiandikisha huku wengi wakisingizia wanafatilia fedha zao za korosho walizouza.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com