Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM Ndg Humphrey Polepole akizungumza wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari kutangaza majina ya wagombea waliopitishwa kugombea Ubunge wa Afrika Mashariki
Na Mwandishi wetu
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndg. John Pombe Magufuli, leo tarehe 29 Machi 2017 ameongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.
Kikao cha Kamati Kuu kimepokea taarifa ya Mchakato wa wanachama na makada wa CCM wanaoomba ridhaa na dhamana ya kuwa Wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
Wajumbe wa Kamati Kuu wametafakari kwa kina wa wameridhishwa na uwazi wa mchakato mzima na namna ambavyo chama kimeonesha demokrasia pana, komavu na shirikishi. Katika mchakato huu jumla ya wanachama na makada 450 walijitokeza, wanawake wakiwa 93 na wanaume 357, wengi wakiwa na elimu ya kuanzia Chuo na Chuo Kikuu.
Chama cha Mapinduzi katika kuzingatia Usawa wa wanawake na wanaume, imefanya uteuzi wa wana CCM 12 kwa mchanganuo wa Bara Me(4) na Ke(4) na Zanzibar Me(2) na Ke(2) ambao majina yao yatawasilishwa Bungeni kwa Uamuzi wa mwisho. Pia chama kimewapa Pongezi sana wana CCM wote ambao wameomba ridhaa
WALIOPATA UTEUZI KUPITIA CHAMA CHA MAPINDUZI(CCM) ILI KUOMBA RIDHAA KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUWA WAJUMBE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI
TANZANIA BARA
WANAWAKE
1.Zainabu Rashid Mfaume KAWAWA
2.Happiness Elias LUGIKO
3.Fancy Haji NKUHI
4.Happiness Ngoti MGALULA
WANAUME
1.Dkt. Ngwaru Jumanne MAGHEMBE
2.Adam Omari KIMBISA
3.Anamringi Issay MACHA
4.Charles Makongoro NYERERE
TANZANIA ZANZIBAR
WANAWAKE
1.Maryam Ussi YAHYA
2.Rabia Abdalla HAMID
WANAUME
1.Abdalla Hasnu MAKAME
2.Mohamed Yussuf NUH
Wednesday, March 29, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu anawataarifu wakazi wa Wilaya hiyo kuwa Mwenge wa Uhuru unataraji kuwasil...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya kilim...
-
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe NEEMA MGAYA (Katikati Mstari wa Mbele) akiwa na baadhi ya wanawake aliowakabidhi vyerehani 370 v...
-
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na viongozi na wataalam wa elimu kuanzia ngazi ya s...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment