Thursday, December 8, 2016
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais,
Mazingira na Muungano January Makamba amesema kuwa mpango wa serikali
ni kuwa na vyanzo vingi vya uzalishaji umeme ili kuwa na vyanzo vya
nchi endelevu na kuunga mkono juhudi za benki ya Dunia kuzalisha umeme
wa upepo katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.
“Kwa kuwa umeme huo utazalishwa kwenye
maeneo ya vijijini, wananchi wanatakiwa kupata umeme kwa bei rahisi
kulingana na uchumi wao na sio kuuziwa umeme kwa bei juu, na zaidi
Wizara yake inapenda kuweka wazi kuwa huu mradi una faida kubwa sana
kulingana na mfumo wa nchi ulivyo,”amesema Makamba.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya
kuzalisha umeme wa upepo Afrika Mashariki Six Telecoms, Rashid Shamte
amesema kuwa mfumo huu wa gridi ndogondogo una faida kubwa sana kwa
wananchi kwani asilimia kubwa kulingana na ripoti ya benki ya dunia
wananunua umeme wa bei nafuu kwahiyo serikali imekubaliana na kampuni
yetu na imeweza kukubali kuwa mradi huu una tija na utasimamiwa na
serikali yenyewe kupitia kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida pamoja na
Halmashauri.
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono Wananchi wa Hai mara baada ya kuwasili Bo...
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
-
WAZOHURU ARUSHA: Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Modestus Mkude amewataka wafanyabiashara Wilayani hapo kushirikiana na Mamlaka ya Mapa...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya kilim...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment