METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, September 18, 2016

Buhari amlaumu mhudumu hotuba yake ilipofanana na ya Obama

Buhari
Bw Buhari amekuwa akiwahimiza raia wa nchi hiyo wabadili tabiaRais wa Nigeria Mohammadu Buhari amemalamu mmoja wa wahudumu wake kwa kuiba sehemu za hotuba ya Rais wa Marekani Barack Obama.

Sehemu kadha za hotuba ya Buhari aliyotoa tarehe 8 mwezi huu zilifanana na sehemu za hotuba ya Obama aliyotoa baada ya kushinda uchaguzi mwaka 2008.

Gazeti la This Day linasema Bw Buhari, kwenye hotuba yake ya Change Begins With Me (Mabadiliko Yanaanza Nami), alitumia maneno sawa na yaliyotumiwa na Bw Obama baada ya kushinda uchaguzi mwaka 2008.

Hotuba ya Bw Buhari ilisoma: "Lazima tujiepushe na vishawishi vya kurejelea mapendeleo, ukosefu wa ustaarabu na ukosefu wa ukomavu ambavyo vimekuwa sumu kwa taifa hili kwa muda mrefu. Tulete moyo mpya wa kuwajibika, moyo wa kutoa huduma, kujitolea na kujitoa mhanga. Sote, tuungane na kufanya kazi kwa bidii na kujali, sio sisi wenyewe tu binafsi bali pia kuwajali wengine.
Bw Obama alisema hivi mwaka 2008, ingawa nukuu zinatoka sehemu tofauti za hotuba yake: „Nawasihi tujiepushe na vishawishi vya kurejelea mapendeleo, ukosefu wa ustaarabu na ukosefu wa ukomavu ambavyo vimekuwa sumu kwa siasa zetu kwa muda mrefu."

"Kwa hivyo, hebu tulete moyo mpya wa uzalendo, wa kuwajibika, ambapo kila mmoja wetu anaamua kuungana na kufanya kazi kwa bidii na kujali sio sisi wenyewe tu binafsi bali pia kuwajali wengine."

Msemaji wa Buhari Garba Shehu anasema kuwa wale waliohusika wataadhibiwa.

Bw Buhari hatakuwa kiongozi wa kwanza mashuhuri kudaiwa kukopa maneno ya hotuba kutoka kwa mtu mwingine.

Wiki chache zilizopita, mke wa mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump, Melania, alidaiwa kukoma sehemu za hotuba yake kutoka kwa hotuba iliyotolewa na mke wa Rais Obama, Michelle, mwaka 2008. 

BBC
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com