METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, February 28, 2016

Yanga yaifumua Cercle de Joachim goli mbili kwa bila, sasa kupambana na APR

Yanga 

Mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania, Yanga SC imefanikiwa kufuzu mzunguko wa pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifunga klabu ya Cercle de Joachim goli mbili kwa bila na hivyo kuwa na wastani wa goli tatu kwa bila ambao unaipa Yanga nafasi ya kusonga mbele.

Magoli ya Yanga katika mchezo huo yamefungwa na Amissi Tambwe katika dakika ya tatu baada ya kuunganisha krosi iliyopigwa na Simon Msuva.

Goli la pili katika mchezo huo lllifungwa na kiungo wa klabu hiyo, Thaban Kamusoko katika dakika ya 56 na hivyo kuihakikishia Yanga nafasi ya kucheza mzunguko wa pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Baada ya ushindi huo, Yanga inataraji kupambana na APR ya Rwanda katika mchezo wa mzunguko wa pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com