METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, February 22, 2016

Shule ya Sekondari Ilboru sasa Kuchuja Wanafunzi


Kufuatia kutofanya vizuri kitaifa katika mtihani wa kidato cha nne, shule ya sekondari ya watoto wenye vipaji maalumu, IIboru itaanza kuwachuja wanafunzi wasio na uwezo wanaopangiwa kusoma shuleni hapo.
 
Mkuu wa shule hiyo, Julius Shula amesema licha ya Ilboru kuwa ya kwanza kwa shule za Serikali nchini, lakini imebaini upungufu katika upatikanaji wanafunzi.
 
Amesema kuna wanafunzi kutoka shule za binafsi wanaopangiwa IIboru, wamebainika hawana uwezo, hivyo kutilia shaka alama walizopata katika mitihani yao ya kuhitimu darasa la saba.
 
“Tayari tumewapa mitihani waliongia kidato cha kwanza, huwezi amini kuna wanafunzi wanapata alama 0, lakini ukifuatilia matokeo ya kuja hapa wana wastani wa alama zaidi ya 200 sasa hili ni tatizo kubwa,” alisema. 
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com