METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, March 23, 2020

Katibu mkuu Wizara ya Kilimo Bw Gerald Kusaya aridhishwa na maendeleo Mradi wa ujenzi wa Vihenge-Babati


Muonekano wa mradi wa Ujenzi wa Vihenge (8) unaotekelezwa Wilayani Babati Mkoani Manyara chini ya Wakala wa hifadhi ya chakula (NFRA)
Katibu mkuu Wizara ya Kilimo Bw Gerald Kusaya akitoka ndani ya moja ya Vihenge pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Kilimo alioambatananao katika ziara yake kujionea maendeleo ya maradi huo.
Katibu mkuu Wizara ya Kilimo Bw Gerald Kusaya akikagua nyumba za ofisi amabazo zitatumika na watendajiwa Wakala wa hifadhi ya chakula (NFRA) mradi huo utakapo kamilika.

Na Innocent Natai, Arusha

Katibu mkuu Wizara ya Kilimo Bw Gerald Kusaya amewapongeza watendaji wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya chakula (NFRA) na mkandarasi wa mradi wa ujenzi wa Vihenge (8) unaofanywa chini ya NFRA Wilayani Babati Mkoani Manyara, kwa ajili ya uhifadhi wa nataka.

Ameyasema hayo alipotembelea katika eneo la ujenzi wa Vihenge hivyo Babati Mkoani Manyara wakati wa kuhitimisha  ziara  yake ya kuzitembelea taasisi za Wizara  ya Kilimo zilizopo Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara, lengo kuu likiwa ni kufahamiana na watumishi wa taasisisi hizo pamoja na kupata taarifa za utendaji kazi wa taasisi hizo.

Akizungumzia ujenzi huo kusaya amesema kuwa mkandarasi wa vihenge hivyo ameonyesha jitihadi kubwa katika kujali muda sambamba na ubora wa vihenge hivyo pamoja na majengo.

“Mimi kama Katibu Mkuu wa Wizara hii ya Kilimo nimetembelea mradi huu wa ujenzi wa vihenge pamoja na majengo, nimeridhishwa na maendeleo ya ujenzi huu mkubwa wito wangu kwa mkandarasi wa ujenzi huu ni kuhakikisha unakamilishwa kwa wakati na ubora unaohitajika” alisema Kusaya

Kusaya ameongeza kuwa mradi huo wa ujenzi wa vihenge utakapokamilika utakuwa na manufaa makubwa kwa taifa katika kuhakikisha kuwa kunakuwepo na uhifadhi mkubwa wa chakula na pindi ambapo kutakuwa na uhaba wa chakula kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya chakula (NFRA) wataweza kusaidia upatikanaji wa chakula kitakachokuwa kimehifadhiwa katika vihenge hivyo.

Aidha, kupitia wasaa huo aliwataka wataalam wa Wizara ya Kilimo kuhakikisha wanatoa elimu ya uhifadhi bora wa mazao ya kilimo ili kuwasaidia wakulima kuepukana na changamoto ya upotevu wa mazao baada ya mavuno sambamba na “Sumukuvu”

MWISHO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com