METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, December 4, 2019

AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MWAKA MMOJA JELA AU FAINI YA MILIONI MBILI KWA KUKUTWA NA VIUATILIFU VISIVYO SAJILIWA



Na innocent Natai, Morogoro

Mahakama ya Wilaya ya  Ifakara Mkoani Morogoro imemuhukumu kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini ya shilingi za kitanzania milioni mbili pamoja na kulipa gharama za kuteketeza viuatilifu alivyo kamatwa  navyo, Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la,Yerusalem Mwamaja miaka 49 (Mhehe) baada ya kupatikana na viuatiliafu ambavyo havijasajiliwa  kinyume na kifungu cha 19 cha Sheria ya Hifadhi ya Mimea Na. 13 ya mwaka, 1997.

Hukumu hiyo imetolewa na  Hakimu Mkazi wa Mahakama hio,Mheshimiwa Binge Njaga Mashabara,baada ya kujiridhisha na hoja za mashahidi pamoja na vielelezo vilivyo tolewa mahakamani na upande wa mashtaka,bila kuacha shaka yeyote.

Hakimu Mashabara alisema vitendo kama hivyo vinawasababisha hasara kwa wakulima na serikali kwa ujumla ukiachilia mbali kuendelea kusababisha madhara kwa mazingira, afya za binadamu, wanyama na mimea. Hivyo alisema anatoa adhabu hiyo ili iwe onyo na fundisho kwa wote wenye tabia kama hizo.

Awali, mwendesha mashtaka,alidai kuwa hakukuwa na kumbukumbu za makosa ya nyuma dhidi ya mshatakiwa huyo,sambamba na hilo na  aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali ili iwe onyo na fundisho kwa wote wenye tabia kama hizo.

Katika maombolezo yake Yerusalem Mwamaja alisema kuwa hakufahamu kama kufanya hivyo ni kosa kisheria na aliomba apunguziwe adhabu kwani ni mara yake ya kwanza kufanya kitendo hicho na hata rudia.

Akizungumzia hukumu hio baada ya kutoka Mahakamani hapo Bw. Solomon Shedrack Mungure ambae ni Mkaguzi wa Viuatilifu kutoka ofisi ya TPRI Dar es Saalam ametoa rai kwa wauzaji na wasambazaji wa Viuatilifu nchi nzima wenye tabia za kuuza na kusambaza viuatilifu ambavyo havija sajiliwa na kukaguliwa na TPRI kuacha mara moja kwani zoezi la ukaguzi na kuwabaini watu kama hao ni endelevu hivyo watakamatwa mara moja na kuwafikisha mahakamani.

Aidha mkaguzi huyo amehitimisha kwa kusema kuwa kuuza au kusambaza viuatilifu bila kuwa na elimu na kibali ni kosa kwani kunaweza kumsababisha madhara kwa msambazaji,muuzaji au mtumiaji hivyo ni vyema kufuata taratibu za kupata kibali ikiwemo kupata mafunzo yanayotolewa na TPRI ya matumizi sahihi na salama ya viuatilifu.

MWISHO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com