METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, March 19, 2019

TUNA FURSA YA ZAO LA MUHOGO – MHE MGUMBA



Na Beatrice Kimwaga, Wizara ya Kilimo-Lindi

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba amewasihi wakulima nchini kulima kwa wingi kilimo cha muhogo kwani kufanya hivyo kutaimarisha kipato chao.

Mgumba ameyasema hayo mara baada ya kutembelea Kiwanda cha kuchakata Muhogo kilichopo katika kijiji cha Mbalala kata ya Mtama katika Halmashauri ya Lindi wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Lindi.

Katika ziara hiyo Mhe Mgumba alikipongeza kiwanda cha Cassava Starch of Tanzania Corporation ( CSTC) kwa kutoa ajira nyingi kwa watanzania walio wengi katika wilaya hiyo sambamba na kuwapongeza kwa uamuzi wao mzuri wa kuwekeza nchini.

Alisema kuwa wawekezaji hao wameunga mkono Rais Dkt John Pombe Magufuli katika azma yake ya kufanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda.

“Kuwepo kwa kiwanda hiki kuna faida kubwa kwani kitatengeneza ajira kwa wananchi kupata soko la muhogo, uzuri ni kwamba kiwanda hiki kitatumia malighafi zinazozalishwa hapa Tanzania na sio nje ya nchi” alisema Mhe. Mgumba

Alisema kuwa pamoja na mambo mengine lakini changamoto kubwa iliyopo ni uwepo wa tija ndogo katika mazao yetu hivyo uwepo wao nchini utasaidia wananchi kujifunza na kupata teknolojia mpya waliyokuja nayo na teknolojia hiyo itasambaa Lindi nzima.

Kwa upande wa wamiliki wa kiwanda hicho wamesema kwamba lengo lao ni kuzalisha tani elfu sitini na kwa upande wa Serikali Mhe. Mgumba amesema  imejipanga kwenda kwenye uchumi wa kati ifikapo 2020.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli imedhamiria kuimarisha masoko ya mazao ya wakulimahivyo wakulima jukumu lao kubwa ni kuongeza uzalishaji na tija katika kilimo.

MWISHO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com