Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza
katika mkutano wa urutubishaji vyakula
Baadhi ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri
Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo
Baadhi ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri
Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi Mhe. Selemani Jafo
amewataka wataalam wa lishe nchini kufikisha elimu ya lishe kwa jamii kwa lugha
nyepesi ya kiswahili katika jamii.
Jafo aliyasema hayo wakati wa ufungaji wa mkutano mkuu wa siku
mbili wa wataalam wa mambo ya lishe uliokuwa ukilenga suala la urutubishaji wa
vyakula hapa nchini.
Mkutano huo wa kitaifa ulifanyikia Dar as salaam katika ukumbi
wa kimataifa wa Nyerere ambapo wataalam wa lishe, watafiti, wadau wa maendeleo,
wamiliki wa Viwanda vya kurutubisha vyakula, pamoja na wananchi walishiriki.
Akizungumza katika mkutano huo, Jafo alitoa angalizo kwa wataalam
na watendaji kutumia lugha isiyo rafiki kwa wananchi (lugha ya kiingereza)
wakati wa kujadili na kufikisha elimu ya lishe.
Jafo amesisitiza matumizi ya lugha ya kiswahili ili wananchi
walengwa wa elimu hiyo waweze kufahamu nini kinajadiliwa na namna ya
utekelezaji wake ili kufanikisha mapambano dhidi ya tatizo la utapiamlo hapa
nchini.
Aidha, Jafo amezitaka taasisi zinazosimamia ubora wa vyakula (
TBS na TFDA) kuongeza ufanisi wa usimamizi wa bidhaa ili viwanda vinavyorutubisha
vyakula vitekeleze wajibu wao na wasisite kuwachukulia hatua wale wote wataokiuka
utaratibu.
Amesisitiza urutubishaji wa chumvi kwa kuweka madini joto
sambamba na urutubishaji wa unga wa mahindi, ngano na mafuta ya kula.
0 comments:
Post a Comment