Msanii
wa Bongo Fleva Nchini Ali Kiba amefunguka juu ya siri inayomfanya awe
anapata mapokezi makubwa kwa mashabiki wake kila anapotoa kazi mpya
kuwa ni kazi nzuri ambazo amekuwa akizifanya.
Akizungumza
Juma tatu hii ndani ya ‘Planet Bongo’ya East Africa Radio,Ali Kiba
alifunguka kuwa kazi nzuri ndio zinazomfanya awe anapata mapokeo makubwa
sana kutoka kwa mashabiki wa muziki wake na wala si kitu kingine kama
ambavyo imezoeleka kwa baadhi ya wasanii walio wengi kutumia ‘kiki’ kwa
ajili ya kupata mapokeo makubwa ya kazi zao.
‘’Mi
nafanya kazi nzuri ndio mana mapokeo ya kazi zangu kwa mashabiki
yanakuwa makubwa na sio kitu kingine ninacho kifanya katika kazi yangu
zaidi ya kufanya kazi nzuri’’alisema Ali kiba.
Ali
Kiba ameanza rasmi kufanya ziara katika vyombo mbali mbali vya habari
kwa ajiri ya kuutambulisha wimbo wake mpya ‘Seduce Me’ ambao unatamba
sana kwa sasa huku akiongozana na mtayarishaji wa kazi hiyo ‘Man Walter’
kutoka katika studio za Combination Sound.
0 comments:
Post a Comment