METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, February 14, 2016

Wahamaiji haramu 15 kutoka Ethiopia wakamatwa Singida


Jumla ya wahamiaji haramu 15 kutoka Ethiopia (walioketi) wakiwa nje ya ofisi ya uhamiaji mkoa mjini Singida,jana.Vijana hao walikuwa njiani wakielekea Afrika kusini kusaka maisha. (Picha na Nathaniel Limu)

Baadhi ya maafisa uhamiaji mkoa wa Singida.

Idara ya uhamiaji mkoa wa Singida, imefanikiwa kukamata vijana wahamiaji haramu 15 kutoka nchini Ethiopia, kwa tuhuma ya kuingia na kuishi nchini bila kuwa na vibali halali.


Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juzi,Afisa Uhamiaji mkoa wa Singida,DCIS Faith Ihano,alisema wahamiaji hao haramu,wamekamatwa Februari, 12 mwaka huu saa 12.00 jioni Unyankindi mjini hapa.

Alisema wahamiaji hao wamekamatwa wakiwa wamefichwa kwenye nyumba ya mtu binafsi Unyankindi mkabala na kota za nyumba za shirika la nyumba taifa (NHC).

“Kwa sasa tunamshikilia mwenye nyumba huyo kwa mahojiano zaidi na pindi upelelezi/uchunguzi utakapokamilika,tutamfikisha mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili ya kupokea na kuhifadhi wahamiaji haramu,” alisema Ihano.

Aidha Afisa huyo alisema katika kipindi kifupi cha kati ya disemba na januari mwaka huu,wamefanikiwa kukamata wahamiaji haramu 30 kutoka Congo, Malawi na Ethiopia.

“Hii biashara haramu ya kusaidia na kuhifadhi raia wa kigeni wanaoingia nchini kinyume na taratibu na sheria,inafanywa na Watanzania wachache,” alifafanua.

Ihano alitumia fursa hiyo kuwaasa Watanzania wachache wanaojihusisha na biashara hiyo haramu,kuacha mara moja,vinginevyo wakibainika,watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Kwa mujibu wa kijana mmoja Mohammed,ambaye ndiye pekee aliyeweza kuongea kwa kiingereza cha kubabaisha,alisema wametoka kwao kupitia Kenya na lengo ni kufika Afrika kusini kusaka maisha bora
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com