Wednesday, June 19, 2019

WAZIRI UMMY AZINDUA MPANGO MKAKATI WA TAIFA WA MASIKIO NA USIKIVU JIJINI DODOMA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu,akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa taifa wa masikio na usikuvu leo jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu,akikata utepe kuashiria  uzinduzi wa mpango mkakati wa taifa wa masikio na usikuvu leo jijini Dodoma.Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu,akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa taifa wa masikio na usikuvu leo jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu,akiwa ameshikiria kitabua akiwaonesha wananchi (hawapo pichani) mara baada ya kuzindua  mpango mkakati wa taifa wa masikio na usikuvu leo jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu,akiwa katika picha ya pamoja  baada ya kuzindua  mpango mkakati wa taifa wa masikio na usikuvu leo jijini Dodoma.

…………………

Na.Alex Sonna,Dodoma

Serikali imezindua mpango mkakati wa taifa wa masikio na usikuvu ambao utasaidia kupeleka  huduma za matibabu ya masikio, pua na koo katika ngazi za chini ili kukabilina na tatizo la usikivu kwa wanachi.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu,akizindua mpango huo jijini Dodoma amesema kuwa  ni lazima watumishi katika ngazi za wilaya ndani ya miezi sita ijayo, wajengewe uwezo ili huduma hizo zipatikane katika ngazi za chini na siyo kusubiri kwenda Muhimbili.

Aidha Waziri Ummy pia amezindua  kambi ya matibabu pamoja na huduma ya uchunguzi wa afya ya sikio unaotolewa na Taasisi ya Starkey hearing Foundation ya nchini Marekani kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania.

Hata hivyo amesema kuwa  pamoja na Serikali kukosa takwimu sahihi za tatizo la usiku nchini lakini pamekuwepo na tafiti ndogondogo ambazo zimekuwa zinafanywa na wadau mbalimbali wa masula hayo.

“Katika tafiti hizo zinaonyesha kuwa asilima 3 ya mwanafunzi wanamatatizo ya kusikia na usikuvu hii inamaanisha kuwa kati ya watoto 100 watatu wanamatatizo ya usikivu”amesema Mhe.Ummy

Amesema kuwa watu wenye magonjwa yasiyo ambukiza kama matatizo ya sukari takwimi zinaonyesha kuwa ni asilimia 24 ambapo kila watu 100 ni watu 24 wenye matatizo ya usikivu.

Kwa upande wa watu wanaofanya kazi katika maeneo ya uchimbahi wa madini na katika viwanda vya kutengeneza nguo ni asilimia 50 ya watu wanamatatizo ya usikivu.

“Kutokana na kutokuwa na wataalamu wa kutosha wa masuala ya masiko nchi yetu imekuwa ikisafirisha watoto kwenda India kila mwaka watoto 13 ambapo mtoto mmoja hutumia fedha kati ya Sh. Milioni 80 hadi 100”amesema Mhe.Ummy

Aidha Mhe.Ummy amewataka wananchi kujijengea tabia ya kwenda kufanya vipimo vya masiko,pua na koo ili kuweza kubaini mataizo kwa wakati.

No comments:

Post a Comment