Saturday, February 9, 2019

WIZARA YAKUTANA NA KAMPUNI ZINAZOKUSUDIWA KUJENGA VINU VYA KUYEYUSHA, KUSAFISHA MADINI


Wataalam wa Wizara ya Madini katika kikao na kampuni  mbalibali  zinayokusudiwa kujenga Vinu vya Kuchenjua,  Kuyeyusha na  Kusafirisha Madini.

Katika jitihada za kuhamasisha shughuli za Uongezaji Thamani Madini Nchini, kuanzia tarehe 6 hadi 7 Februari, 2019, Wizara ya Madini ilikutana na baadhi ya Kampuni zinazokusudiwa kujenga Vinu vya Kuchenjua, Kuyeyusha na Kusafisha Madini nchini.

Lengo la wizara kukutana na kampuni hizo ilikuwa ni kuangalia uwezo wa kifedha, tekinolojia na Utayari wao. Kampuni hizo ni kutoka Ndani na Nje ya Nchi.

Serikali inahamasisha shughuli za uongezaji Thamani madini kufanyika nchini ili kuongeza pato, ajira na uhuishaji wa tekinolojia kwa wazawa.

No comments:

Post a Comment